-
Jihadul-Islami: Muqawama hautaitambua Israel, hakutakuwa na suluhu bila Palestina kupata haki zake
Nov 15, 2025 22:59Mwakilishi wa harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina hapa mjini Tehran amesema: "sisi katika mavuguvugu ya Muqawama wa Kiislamu hatutambui uwepo wa utawala wa Kizayuni na hatulazimiki kuutambua, hasa kwa vile utawala huu hautambui hata uwepo wa watu wa Palestina."
-
Maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la kizayuni zagunduliwa Ghaza
Nov 14, 2025 04:13Timu za uokoaji za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimegundua na kufukua maiti zingine 51 za Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Maafa ya vita vya kinyama vya Israel yamepelekea Wapalestina 6,000 wa Ghaza kukatwa viungo
Nov 13, 2025 23:07Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Ghaza imetoa ripoti inayoonyesha kuwa, Wapalestina 6,000 wamekatwa viungo katika eneo hilo tangu utawala wa kizayuni wa Israael ulipoanzisha vita vya kinyama Oktoba 2023 ambavyo vimeendelea kwa muda wa miaka miwili.
-
UN: Raia 114 wameuawa Lebanon katika ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa na Israel
Nov 13, 2025 23:07Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa Israel uliotokana na makubaliano yaliyofikiwa kati ya utawala huo wa kizayuni na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon ya Hizbullah mnamo Novemba 2024 umesababisha vifo vya raia 114 wa nchi hiyo.
-
Mgogoro wa kisaikolojia miongoni mwa wanajeshi wa Israel; Wizara ya Vita ya Israel: Kujiua wanajeshi ni kielelezo cha kushindwa
Nov 13, 2025 22:54Gazeti la Uingereza The Independent, limeashiria ongezeko la kiwango cha kila mwaka cha kujiua katika jeshi la Israel baada ya vita vya Gaza, na kuandika kuwa: "Zaidi ya wanajeshi 11,000 wa Israel wamekumbwa na aina mbalimbali za matatizo ya kisaikolojia baada ya vita hivyo, na takwimu kuhusu wanajeshi wanaojiua baada ya kuondoka jeshini hazijachapishwa."
-
Kujiunga Wazungu na harakati ya kuisusia Israel; mabadiliko ya kweli au mashinikizo ya umma?
Nov 12, 2025 23:05Harakati ya kususia bidhaa za Israeli (BDS) inazidi kupata nguvu kote duniani, tena kwa kasi kubwa, na watu binafsi na taasisi mbalimbali kote ulimwenguni zinajiunga nayo kwa lengo la kuongeza mashinikizo kwa Israel. Katika uamuzi muhimu zaidi wa hivi karibuni, ni nchi ya Ulaya ya Uholanzi kutangaza kwamba inaandaa sheria ya kupiga marufuku kuingiza nchini humo bidhaa zinazozalishwa katika vitongoji haramu vya walowezi wa Kizayuni huko Palestina.
-
Hatari ya ushawishi wa Israel barani Afrika; Tishio lililofichika kwa uhuru wa bara Afrika
Nov 10, 2025 09:35Katika juhudi zake za kuitoa Israel kwenye hali ya kutengwa, Isaac Herzog, rais wa utawala wa Kizayuni wa Israel, anatarajiwa kuelekea barani Afrika.
-
New York Times: Katika vita vijavyo, Iran itarusha makombora 2,000 kwa wakati mmoja kuilenga Israel
Nov 10, 2025 02:49Gazeti la The New York Times la nchini Marekani limetahadharisha kwamba ikiwa Israel itaishambulia tena Iran, Tehran itajibu hujuma hiyo kwa nguvu zaidi, kwa kurusha makombora 2,000 kwa wakati mmoja kuulenga utawala huo wa kizayuni.
-
HAMAS: Lengo la safari ya rais wa Israel Afrika ni kubadilisha misimamo ya nchi zinazounga mkono Palestina
Nov 10, 2025 02:48Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa safari ya rais wa utawala ghasibu wa kizayuni katika nchi za Afrika ni jaribio la kutaka kubadilisha msimamo wa nchi hizo wa zinazopinga ukoloni na kuunga mkono haki za watu wa Palestina.
-
Katz amtusi vikali Erdogan baada ya mahakama ya Uturuki kutoa hati za kukamatwa viongozi 37 wa Israel
Nov 10, 2025 02:47Waziri wa vita wa utawala wa kizayuni wa Israel, Yisrael Katz amemshambulia kwa matusi makali Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan baada ya mahakama ya nchi hiyo kutoa hati za kukamatwa viongozi 37 wa utawala huo ghasibu kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya kimbari ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.