-
Mabomu ni ghali, risasi ni bei nafuu! Mkakati wa Marekani na Israel wa kuwaua Wapalestina katika safu za chakula
Jul 16, 2025 13:20Katika mwezi wa 23 wa Vita vya Gaza, ambapo utawala wa Kizayuni wa Israel umefanya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza kwa ukatili na unyama wa hali ya juu na kwa kutumia silaha ya njaa, sasa utawala huo umebuni mbinu mpya kwa ajili ya kile kinachojulikana kama 'mauaji ya bei nafuu' ya wakazi wa Gaza.
-
Kamanda wa ulinzi wa anga wa Israel abadilishwa kutokana na kipigo cha makombora cha Iran
Jul 16, 2025 10:22Kamanda wa kikosi cha ulinzi wa anga cha jeshi la Israel amebadilishwa kufuatia mashambulizi ya hivi karibuni ya makombora ya Iran yaliyolenga maeneo ya Palaestina yanayokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
"Marubani 30 wa Israel waliuawa katika operesheni ya kulipiza kisasi ya Iran"
Jul 16, 2025 07:29Balozi wa zamani wa Iran nchini Iraq amefichua kuwa, marubani 30 wa Israel waliuawa wakati wa moja ya operesheni za kulipiza kisasi za Iran katika vita vya siku 12, akisisitiza kuwa hili lilikuwa pigo kubwa kwa utawala wa Kizayuni.
-
Wanajeshi wengine 4 wa Israel waangamizwa katika mashambulizi tofauti Gaza
Jul 14, 2025 12:30Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti habari ya kuangamizwa wanajeshi wanne wa Kizayuni katika mashambulizi tofauti katika Ukanda wa Gaza jana Jumatatu.
-
Waliouawa shahidi Ghaza wapindukia 58,000, Israel yaendeleza mashambulizi ya kinyama bila ya khofu
Jul 14, 2025 00:38Wapalestina wasiopungua 58,026 wameshuawa shahidi katika vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Gaza tangu Oktoba 2023.
-
Olmert: Walowezi haramu wanafanya 'uhalifu wa kivita' Ufukwe Magharibi kwa uungaji mkono wa utawala
Jul 13, 2025 14:03Waziri mkuu wa zamani wa utawala wa kizayuni Israel Ehud Olmert amekiri kuwa walowezi haramu wa kizayuni wamekuwa wakifanya "uhalifu wa kivita" kila leo dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu huku wakilindwa na utawala wa Tel Aviv.
-
Mabalozi wa nchi 28 wakagua jengo la IRIB lililoshambuliwa na jeshi la kizayuni
Jul 13, 2025 12:10Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB), Peyman Jebelli, amewapokea mabalozi wanaowakilisha nchi 28 hapa mjini Tehran waliofanya ziara ya kukagua moja ya majengo ya IRIB lililolengwa na shambulio la kigaidi la jeshi la utawala wa kizayuni Israel mwezi uliopita.
-
Wabunge wa Iran waandaa muswada wa kuimarisha vikosi vya ulinzi kwa vita kamili na Israel
Jul 13, 2025 10:46Wabunge wa Iran wamo mbioni kuandaa mswada wa kuongeza bajeti ya matumizi ya kijeshi kwa lengo la kuviimarisha Vikosi vya Ulinzi kwa ajili ya makabiliano ya kijeshi ya pande zote na utawala haramu wa kizayuni wa Israel.
-
Netanyahu: Ni kweli tuliwaua kigaidi wanasayansi wa nyuklia wa Iran
Jul 13, 2025 03:27Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekiri kwamba utawala huo wa Kizayuni uliwaua kwa utaratibu maalum wanasayansi wa nyuklia wa Iran.
-
Nini madhumuni ya barua mpya ya Iran kwa Baraza la Usalama kuhusiana na uvamizi wa kijeshi wa Israel dhidi ya Iran?
Jul 12, 2025 23:05Amir Saeid Iravani Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amemuandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama la umoja huo, na kuwasilisha ripoti iliyosasishwa kuhusu uharibifu uliosababishwa na uvamizi mkubwa wa kijeshi na wa bila ya sababu wa utawala wa Israel dhidi ya Iran.