-
Hillary Clinton: Marekani inapasa kurejea katika makubaliano ya JCPOA
Aug 18, 2020 02:26Waziri wa zamani wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani amesisitiza kuwa serikali ijayo ya nchi hiyo inapasa kurejea katika mapatano ya JCPOA; kwa sababu hatua hiyo ni kwa maslahi ya Washington.
-
Onyo la Rouhani kuhusu JCPOA; Ulaya isitumbukie kwenye mtego wa Marekani
Aug 13, 2020 04:54Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa azimio lilopendekezwa na Marekani katika Barazala Usalama la Umoja wa Mataifa linakiuka moja kwa moja azimio nambari 2231 la baraza hilo na hivyo kuzitaka nchi zote na hasa zilizotia saini mapatano ya kimataifa ya nyuklia ya JCPOA, zilipinge.
-
Araqchi: Iran haitaacha haki yake isiyo na shaka kwa sababu tu ya ubabe wa Marekani
Jul 26, 2020 23:11Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema, kutumia nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani ni haki ya wazi na isiyo na shaka ya wananchi wa Iran na akasisitiza kuwa: Licha ya kuitolea gharama kubwa kutokana na vikwazo, Jamhuri ya Kiislamu haitaiacha haki yake hiyo ya wazi kabisa kwa sababu tu ya ubabe wa Marekani.
-
Sisistizo la Borrell kuhusu kulindwa JCPOA; nara isiyotekelezeka kivitendo
Jul 20, 2020 02:17Umoja wa Ulaya (EU) na Troika ya Ulaya inayoundwa na Ujerumani, Ufaransa na Ujerumani ni pande zilizokuwa na nafasi muhimu katika kufikiwa mapatano ya nyuklia ya Iran maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA).
-
Borrell: Mapatano ya Trump hayawezekani, JCPOA ilindwe
Jul 19, 2020 08:08Mkuu wa Siasa za Nje wa Umoja wa Ulaya kwa mara nyingine tena amesisitizia udharura wa kulindwa na kuheshimiwa makubaliano ya nyuklia ya Iran yanayofahamika kwa kifupi kama JCPOA, na kueleza bayana kuwa ni jambo lisiloyumkinika kufikiwa kile kinachoitwa "Mapatano ya Tump."
-
Russia na Ujerumani: Vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran havina maana
Jul 16, 2020 03:24Rais wa Russia na Kansela wa Ujerumani wamesisitiza kuwa, vikwazo vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran havina umuhimu wowote.
-
Rais Rouhani: Iran katu haitasalimu amri kwa mashinikizo ya madola makubwa hasa Marekani
Jul 15, 2020 08:28Rais Hassan Rouhani amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu katu haitasalimu amri kwa mashinikizo ya madola makubwa na hasa Marekani na akaongeza kwamba: Marekani ijue kwamba, kamwe haitafikia malengo yake licha ya hatua zake haribifu inazochukua dhidi ya maslahi ya taifa la Iran.
-
Zarif: Marekani inadhalilisha sheria na diplomasia na kuhatarisha usalama wa dunia
Jul 14, 2020 22:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametuma ujumbe kwa mnasaba wa mwaka wa tano wa kufikiwa mapatano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji (JCPOA) na kusema: "Kitendo cha Marekani cha kudhalilisha sheria na udiplomasia ni jambo linalohatarisha usalama wa nchi hiyo na dunia kwa ujumla mbali na kuchafua jina la Washington katika uga wa kimataifa."
-
Mousavi: Vikwazo vya silaha dhidi yake vikirefushwa, Iran itatoa jibu kali
Jul 10, 2020 20:13Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema iwapo vikwazo vya silaha dhidi ya Iran vitarefushwa kufuatia mashinikizo ya Marekani basi Jamhuri ya Kiislamu itatoa jibu kali na muafaka.
-
Zarif: EU inapaswa kufungamana na wajibu wake katika mapatano ya JCPOA
Jul 06, 2020 22:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema nchi za Umoja wa Ulaya zinapaswa kufungamana na wajibu wake katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia ya JCPOA.