-
Iran hufanya majaribio zaidi ya 40-50 ya makombora kila mwaka
Dec 11, 2018 21:42Kamanda wa Kitengo cha Angani cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, IRGC, amezungumzia habari kuhusu Iran kufanya jaribio la kombora la balistiki hivi karibuni na kusema: "Kauli za wakuu wa Marekani ni ishara kuwa, wanalipa umuhimu mkubwa sana suala la majaribio hayo."
-
Korea Kusini yakadhibisha ripoti ya taasisi ya kifikra ya Marekani kuhusu Korea Kaskazini
Nov 13, 2018 11:13Ofisi ya Rais Moon Jae-in wa Korea Kusini imekadhibisha ripoti ya taasisi ya kifikra ya Marekani ya 'Kituo cha Utafiti wa Kimataifa na Kistratijia' juu ya kuendelea shughuli za makombora ya siri ya Korea Kaskazini.
-
Nasrullah: Kuwa na uhusiano wa kawaida na Israel kunafichua sura halisi za wanafiki
Nov 11, 2018 01:08Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kwamba, kuwa na uhusiano wa kawaida nchi za Kiarabu na utawala haramu wa Israel kutafichua sura halisi za wanafiki na wahadaaji.
-
Yemen yaipiga Saudia kwa kombora la balestiki baada ya wavamizi hao kuua Wayemen 8 wa familia moja
Nov 08, 2018 11:18Jeshi la Yemen likishirikiana na wapiganaji wa Kamati za Kujitolea za Wananchi, limevurumisha kombora la balestiki lililotengenezwa nchini humo na kupiga kambi ya mamluki wa Saudi Arabia, katika mkoa wa kaskazini mwa nchi hiyo wa Jawf, na kuangamiza mamluki kadhaa.
-
Uwanja wa ndege wa Tripoli, Libya walengwa kwa kombora
Sep 12, 2018 03:09Duru za habari leo asubuhi zimeripoti kuwa uwanja wa ndege wa Tripoli mji mkuu wa Libya umeshambuliwa kwa kombora.
-
Hizbullah kwa mara ya kwanza imezindua aina mbalimbali za makombora yake
Aug 19, 2018 10:51Harakati ya Hizbullah ya Lebanon kwa mara ya kwanza ilipanga kuzindua leo Jumapili sehemu ya makombora yaliyotumiwa na harakati hiyo ya muqawama wa Kiislamu kwa ajili ya kuilinda nchi hiyo katika miaka ya karibuni.
-
Jinamizi la kuendelea kupigwa Saudia kwa makombora ya Wayemen
Jun 13, 2018 02:07Turki al Maliki, msemaji wa muungano vamizi wa Saudi Arabia dhidi ya Yemen ametangaza kuwa hadi sasa Wayemen wameshavurumisha makombora 149 upande wa Saudia.
-
Makombora ya Yemen yaulenga mji mkuu wa Saudia, Riyadh
May 09, 2018 21:56Wanajeshi wa Yemen wametumia makombora yaliyoundwa nchini humo kushambulia maeneo kadhaa ya kijeshi na kiuchumi ya Saudia Arabia ukiwemo mji mkuu wa nchi hiyo, Riyadh.
-
Syria: Hivi sasa tuna uwezo mkubwa wa kutungua makombora ya adui
Apr 17, 2018 09:51Mshauri wa Rais Bashar al-Assad wa Syria, Bouthaina Shaaban amesema kuwa, jeshi la Syria limethibitisha uwezo mkubwa wa makombora yake hasa baada ya kukabiliana vilivyo na shambulizi la hivi karibuni la Marekani, Uingereza na Ufaransa dhidi ya nchi hiyo.
-
Jeshi la Syria latungua makombora 9 yaliyolenga viwanja vya ndege vya kijeshi
Apr 16, 2018 23:18Jeshi la Syria mapema leo asubuhi limetungua makombora tisa ambayo yalikuwa yamelenga viwanja vya ndege vya kijeshi vya Shayrat mkoani Homs na Al Dumayr katika viunga vya mji mkuu Damascus.