Pars Today
Korea Kaskazini imekosoa sababu iliyotolewa na Marekani ya kutaka kuitishwa kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kujadili jaribio la kombora la hivi karibuni lililofanywa na serikali ya Pyongyang.
Korea Kaskazini imetangaza kufanya kwa mafanikio 'jaribio jingine muhimu' katika Kituo cha Kurushia Satalaiti cha Sohae siku ya Ijumaa.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini imesema kuwa, Marekani haina kitu kipya inachoweza kukiwasilisha kwenye mazungumzo na serikali ya Pyongyang.
Mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema haiwezekani kupatikana amani katika Rasi ya Korea kupitia njia ya vikwazo na mashinikizo na kwamba, vikwazo haviwezi kuchukua nafasi ya udiplomasia na njia ya utatuzi wa kisiasa.
Jeshi la Korea Kusini limetangaza kwamba Korea Kaskazini imelifanyia majaribio kombora lake jipya la balestiki.
Kim Jong-un Kiongozi wa Korea Kaskazini ametembelea taasisi za kijeshi za nchi hiyo katika maeneo ya mpakani na kulitaka jeshi kujiweka tayari kukabiliana na vitisho vyovyote vya adui.
Serikali ya Korea Kaskazini imetoa onyo jipya kwa viongozi wa Marekani kwamba, iwapo nchi hiyo kwa kushirikiana na Korea Kusini zitafanya maneva ya kijeshi, basi Pyongyang itajibu hatua hizo za uhasama.
Mkuu wa kitengo cha masuala ya Marekani katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kaskazini, ameelezea uwezekano wa kuvunjika kikamilifu mazungumzo kati ya Washington na Pyongyang, kutokana na ukwamishaji mambo wa Marekani.
Kiongozi wa Korea Kaskazini amekemea uhasama wa vikwazo na mashinikizo ya Marekani dhidi ya nchi yake na kusisitiza kwamba, kamwe serikali ya Pyongyang haitosalimu amri mbele ya Washington.
Serikali ya Korea Kaskazini imeionya Marekani na baadhi ya nchi za Ulaya juu ya hatua yao ya kuwasilisha suala la majaribio ya makombora yake mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.