Oct 03, 2019 04:13
Mwakilishi wa Korea Kaskazini katika Umoja wa Mataifa amesema, kuhalifu Marekani ahadi zake ndiko kulikosababisha kusita mazungumzo ya nyuklia kati ya nchi mbili. Akihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Kim Song amebainisha kuwa: Hali ya mambo katika Rasi ya Korea ingali inazidi kutokota joto la mivutano, suala ambalo limetokana na hatua za kichochezi za kijeshi na kisiasa za Marekani.