-
'Kulifufua genge la kigaidi la Daesh ndilo lengo la kiistratijia la Marekani'
Feb 25, 2021 23:20Mbunge wa zamani wa Lebanon amesisitiza kuwa, suala la kulifufua genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) ndilo lengo la kiistratijia la Marekani kwani inaamini kwamba genge hilo ni turufu ya kufanikisha malengo yake haramu katika eneo hili.
-
Wananchi Marekani hawaridhishwi serikali yao kupuuza suala la umaskini
Feb 25, 2021 00:20Utafiti mpya wa maoni nchini Marekani unaonyesha kuwa, akthari ya wananchi hawaridhishwi na hatua ya serikali ya nchi hiyo ya kupuuza vita dhidi ya umaskini, kuboresha huduma za afya na elimu.
-
Wahanga nusu milioni wa virusi vya corona nchini Marekani, sababu na taathira zake
Feb 23, 2021 23:11Baada ya kupita mwaka mmoja sasa tangu kulipotokea mlipukowa ugonjwa wa Covid-19 nchini Marekani na kufeli kwa serikali ya nchi hiyo katika kukabiliana na janga hilo, sasa idadi ya wahanga wa corona imepindukia watu nusu milioni kwa kadiri kwamba, Rais Joe Biden amemuru bendera za nchi hiyo zipepee nusu mlingoti.
-
Caracas yajibu vikwazo vya Marekani na waitifaki wake dhidi ya Venezuela
Feb 23, 2021 09:40Viongozi wa Caracas wamelaani "vita vya kiuchumi vya pande kadhaa" za Umoja wa Ulaya na Marekani dhidi ya Venezuela.
-
Hizbullah yasema itaendelea kusimama na Iran mkabala wa Marekani
Feb 21, 2021 04:12Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema harakati hiyo ya muqawama itaendelea kusimama bega kwa bega na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kukabiliana na Marekani.
-
Trump aliacha kwa makusudi maambukizo ya corona yaongezeke Marekani baada ya kubwagwa katika uchaguzi
Feb 21, 2021 00:44Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa la Magonjwa ya Kuambukiza ya nchini Marekani amesema kuwa, rais wa zamani wa nchi hiyo Donald Trump aliacha kwa makusudi maambukizo ya ugonjwa wa COVID-19 yaongezeke nchini humo baada ya kubwagwa katika uchaguzi wa Novemba 3, 2020.
-
Morocco yashadidisha ukandamizaji baada ya kuanzisha uhusiano na Israel
Feb 20, 2021 09:15Serikali ya Morocco imeshadidisha mbinyo, ukandamizaji na ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya wanaharakati na wananchi wa kawaida nchini humo, baada ya Rabat kukubaliana na utawala wa Kizayuni wa Israel kuanzisha uhusiano wa pande mbili.
-
Khatibzadeh: Ili kuhuisha JCPOA, ni dharura Marekani kuondoa kivitendo vikwazo dhidi ya Iran
Feb 19, 2021 23:44Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema njia pekee ya kuhuisha mapatano ya nyuklia ya JCPOA ni Marekani kuondoa vikwazo dhidi ya Iran.
-
Wabunge wa Iraq wataka uingiliaji wa Marekani katika masuala ya nchi hiyo ukomeshwe
Feb 19, 2021 10:33Wabunge kadhaa wa Iraq wametoa indhari kuhusu uingiliaji wa Marekani hasa katika kadhia ya uchaguzi ujao wa bunge na katika masuala ya kijeshi na kiusalama ya nchi hiyo.
-
Biden akiri, ubaguzi wa rangi unaendelea kuitafuna jamii ya Marekani
Feb 19, 2021 04:38Ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa kimbari na ukatili dhidi ya watu weusi daima vimekuwa miongoni mwa sifa kuu za jamii ya Marekani tangu nchi hiyo ilipoasisiwa, na hadi sasa Wamarekani weusi wangali wanasumbuliwa na aina mbalimbali za ubaguzi na ukatili.