-
Rouhani: Kutengwa zaidi, matunda ya mashinikizo ya juu zaidi ya Marekani dhidi ya Iran
Sep 20, 2020 23:47Rais Hassan Rouhani ameashiria kuhusu kugonga mwamba njama za Marekani dhidi ya taifa la Iran na kueleza bayana kuwa: Hatua za Washington mkabala wa Iran hazijakuwa na matokeo mengine isipokuwa kuifanya nchi hiyo itengwe zaidi katika uga wa kimataifa.
-
Bin Zayed aishauri Pentagon ikihamishie Imarati kituo cha kijeshi cha Incirlik kilichoko Uturuki
Sep 20, 2020 23:46Baadhi ya duru zimeripoti kuwa mrithi wa ufalme wa Abu Dhabi Mohammad bin Zayed amefanya mashauriano na Wizara ya Ulinzi ya Marekani Pentagon juu ya mpango wa kukihamishia Imarati kituo cha anga cha jeshi la Marekani cha Incirlik kilichoko nchini Uturuki.
-
Khatibazadeh: Marekani inajua madai yake ya vikwazo dhidi ya Iran ni hewa
Sep 20, 2020 22:56Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amesema tangazo la Marekani kwamba vikwazo vyote vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Tehran ambavyo vilikuwa vimeondolewa eti vimerejeshwa upya ni madai hewa, yasio na athari yoyote na yaliyo kinyume cha sheria.
-
Vurugu na machafuko Asia Magharibi; natija ya sera za Marekani
Sep 20, 2020 22:56Marekani kwa mara nyingine tena imetoa taarifa ikiituhumu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwamba, eti inazusha vurugu na machafuko katika eneo la Asia Magharibi.
-
Madai ya Marekani kuhusu kurejeshwa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran; ndoto na kujidanganya kwake
Sep 20, 2020 05:56Kugonga mwamba Marekani katika juhudi zake za kutaka muda wa vikwazo vya silaha dhidi ya Iran uongezwe katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kuliifanya serikali ya Donald Trump sambamba na kuibuka na madai kuwa, ni mwanachama wa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kwamba, Iran imekiuka makubaliano hayo, ilidai kurejea upya vikwazo vya kimataifa dhidi ya Tehran na ikatoa muhula wa mwezi mmoja katika uwanja huo
-
Yaliyomo kwenye mpango wa Marekani wa kutaka kumuengua Mahmoud Abbas
Sep 20, 2020 03:31David Friedman, Balozi wa Marekani katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) Alhamisi iliyopita alisema kuwa; Marekani inafikiria kumweka Mohammed Dahlan, kiongozi wa zamani wa harakati ya Fat-h kwenye uongozi wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina kuchukua nafasi ya Mahmoud Abbas, rais wa sasa wa mamlaka hiyo.
-
Marekani yaendelea kupora mafuta ya Syria, malori 30 yahamishiwa Iraq
Sep 20, 2020 03:17Shirika rasmi la habari la Syria SANA limeripoti kuwa, askari wa jeshi la kigaidi la Marekani wameiba malori 30 ya mafuta ya nchi hiyo na kuyahamishia nchi jirani ya Iraq.
-
Biden amtaka Trump ang'atuke madarakani
Sep 20, 2020 02:49Mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democrat amemtaka rais wa nchi hiyo Donald Trump ang'atuke madarakani kwa sababu ya uongozi mbovu alioonyesha katika kukabiliana na virusi vya corona.
-
Vyombo vya Usalama Afrika Kusini: Hakuna ushahidi wa madai ya US dhidi ya Iran
Sep 19, 2020 08:26Idara ya Usalama wa Taifa ya Afrika Kusini imesema hakuna ushahidi wowote iliyoupata wa madai ya Marekani kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inapanga kumuua Lana Marks, Balozi wa Marekani katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.
-
Ufaransa yakadhibisha madai ya Marekani dhidi ya Hizbullah
Sep 19, 2020 08:19Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa imesema hakuna ushadidi wowote unaoonyesha kuwa tawi la kijeshi la harakati ya Hizbullah ya Lebanon limefanya magendo ya kemikali kwa ajili ya kutengeneza mada za mlipuko nchini Ufaransa, kama inavyodai Marekani.