-
Hizbullah: Marekani ndiyo sababu ya matatizo yote ya Lebanon
Jan 26, 2020 09:26Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema Marekani ndiyo chimbuko la matatizo yote yanayoikabili Lebanon.
-
Maveterani wa kivita Marekani wamtaka Trump aombe radhi kwa kudharau hasara kubwa iliyosababishwa na kipigo cha Iran
Jan 25, 2020 23:50Kundi moja la maveterani wa vita vya nje ya Marekani wamemtaka rais wa nchi hiyo Donald Trump aombe radhi kwa kudharau madhara waliyopata wanajeshi wa Marekani baada ya kambi yao ya Ain al Assad ya nchini Iraq kushambuliwa kwa makumi ya makombora ya Iran.
-
Pentagon yakiri tena: Makumi ya askari wa Marekani walipatwa na madhara katika shambulio la makombora la Iran
Jan 25, 2020 23:21Alfajiri ya Jumatano Januari 8 mwaka huu Iran ilishambulia kwa makombora kambi ya jeshi la Marekani ya Ain al Asad huko Iraq ikiwa ni katika kutimiza ahadi yake ya kulipiza kisasi kikali cha mauaji ya kigaidi yaliyofanywa na serikali ya Trump dhidi ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani na wenzake huko Baghdad.
-
Wamarekani waunga mkono mpango wa kumshtaki Trump ICC
Jan 25, 2020 08:09Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa hivi karibuni nchini Marekani unaonesha Wamarekani wanaunga mkono mpango wa kushtakiwa rais wa nchi hiyo, Donald Trump kwa kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani.
-
Idadi ya askari wa Marekani waliojeruhiwa katika jibu la Iran 'yaongezeka'
Jan 25, 2020 04:04Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) imesema makumi ya askari wa nchi hiyo walijeruhiwa na kupatwa na matatizo ya kisaikolojia kufuatia shambulizi la makombora la Iran dhidi ya kambi mbili za kijeshi za nchi hiyo huko Iraq mapema mwezi huu, licha ya utawala wa Washington hapo awali kudai kuwa hakuna askari wake hata mmoja aliyeuawa au kujeruhiwa katika majibu hayo makali ya ulipizaji kisasi yaliyotolewa na Iran.
-
Russia yapinga vikali vitisho vya Marekani vya kumuua kigaidi Brig. Jen. Qaani
Jan 24, 2020 13:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amelaani vitisho vilivyotolewa na Marekani vya kumuua kigaidi kamanda mpya wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (Sepah).
-
Iraq yasubiri kushuhudia tukio la kihistoria; Mapinduzi ya Ishiri ya pili
Jan 24, 2020 04:45Huku Wairaki wakiwa wanasubiri kushuhudia maandamano makubwa ya mamilioni ya watu dhidi ya uwepo wa kijeshi wa Wamarekani katika ardhi ya nchi hiyo, makundi mbalimbali ya Wairaki wanayataja maandamano hayo kuwa 'Mapinduzi ya Ishirini' ya pili.
-
Chris Murphy akosoa kitendo cha Trump kusema uongo kuhusu hasara iliyotokana na shambulio la Iran Ain Assad
Jan 23, 2020 23:22Chris Murphy, Seneta wa Marekani amesema kuwa hadi sasa Rais Donald Trump wa nchi hiyo ameendelea kuwahadaa Wamarekani kuhusu hasara iliyotokana na shambulio la makombora ya Iran kwenye kambi yake ya jeshi ya Ain Assad nchini Iraq.
-
Matokeo hasi ya chokochoko za Marekani Asia Magharibi
Jan 23, 2020 23:22Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa hatua na chokochoko za kijeshi zinazofanywa na Marekani katika eneo la Asia Magharibi, ndio chanzo cha machafuko ndani ya eneo hilo na ameongeza kuwa, uthibitisho wa mwisho wa jambo hilo ni kumuua kigaidi Luteni Qassem Soleimani katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Baghadad, Iraq.
-
Msimamo wa Ulaya kuhusu JCPOA, sera ya mielekeo kinzani yenye hatima moja
Jan 23, 2020 08:30Hatua ya hivi karibuni ya troika ya Ulaya inayozijumuisha nchi za Ujerumani, Ufaransa na Uingereza ya kuanza kutekeleza utaratibu wa kutatua tofauti ndani ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA, ambayo imeanzishwa kwa mashinikizo ya Marekani, imekabiliwa na radiamali kali ya Iran.