-
China yatoa radiamali yake baada ya Marekani kuwatimua wanadiplomasia wake kutoka Washington
Dec 17, 2019 22:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China sambamba na kukosoa vikali hatua ya Marekani ya kuwatimua wanadiploamasia wake kutoka Washington, imeitaka White House kuangalia upya msimamo wake huo ili izuie kuharibika zaidi uhusiano wa nchi mbili.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Lebanon aunga mkono misimamo ya Hizbullah
Dec 17, 2019 09:12Waziri wa Mambo ya Nje wa Lebanon Gebran Bassil ameunga mkono misimamo ya harakati ya muqawama ya Hizbullah katika uga wa kisiasa na kijeshi wa nchi hiyo.
-
Uturuki kujibu mapigo kwa kutambua kuuliwa wakazi wa asili wa Marekani kuwa ni 'mauaji ya kimbari'
Dec 17, 2019 09:11Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema, nchi yake itachukua hatua ya kuyatambua mauaji ya mamilioni ya wakazi wa asili wa Marekani kuwa ni "mauaji ya kimbari" ili kujibu mapigo kwa hatua ya karibuni iliyochukuliwa na serikali ya Washington ya kuyaelezea mauaji ya halaiki ya Waarmenia yaliyofanywa na utawala wa zamani wa Uturuki wa Dola la Othmaniya kuwa ni mauaji ya kimbari.
-
Rais Bashar al Assad: Mapambano dhidi ya magaidi ni utangulizi wa mapambano dhidi ya Marekani
Dec 16, 2019 09:13Rais Bashar al Assad wa Syria amesema kuwa mapambano dhidi ya magaidi ni utangulizi wa makabiliano ya uwepo haramu wa askari wa Marekani nchini humo.
-
Kusitishwa vita vya kibiashara kati ya China na Marekani
Dec 15, 2019 08:24Hatua ya Marekani na China kutangaza kufikiwa makubaliano ya awali ya kibiashara, imesitisha vita vya kibiashara kati ya pande mbili.
-
Waziri Mkuu wa Malaysia: Vikwazo vya US dhidi ya Iran ni haramu
Dec 15, 2019 04:19Waziri Mkuu wa Malaysia amesema vikwazo vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni batili na vya kidhalimu, na ambavyo vinakiuka Mkataba wa Umoja wa Mataifa na sheria za kimataifa.
-
Radiamali ya Korea Kaskazini kwa takwa la Marekani la kuitishwa kikao cha Baraza la Usalama
Dec 15, 2019 03:32Korea Kaskazini imekosoa sababu iliyotolewa na Marekani ya kutaka kuitishwa kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kujadili jaribio la kombora la hivi karibuni lililofanywa na serikali ya Pyongyang.
-
Harakati ya Answarullah ya Yemen: Marekani ndio inazuia kusimamishwa vita
Dec 14, 2019 21:43Mohammed Ali al-Houthi, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mapinduzi nchini Yemen ameitaja Marekani kuwa ndio kizuizi kikuu cha kutosimamishwa uvamizi na mzingiro dhidi ya taifa hilo la Kiarabu.
-
Rais: Zimbabwe haitarejea katika matumizi ya sarafu ya dola ya Marekani
Dec 14, 2019 03:58Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amesema licha ya nchi hiyo ya kusini mwa Afrika kukabiliwa na mtikisiko mkubwa wa kiuchumi, lakini haitarejea katika matumizi ya sarafu ya dola ya Marekani.
-
Nasrullah: Hizbullah ni tishio kubwa kwa njama za Marekani na Israel
Dec 14, 2019 03:55Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema njama ghalati za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel katika eneo zimekuwa zikigonga mwamba kutokana na uwepo na kusimama kidete harakati hiyo ya muqawama.