-
Umoja wa Ulaya wapinga hatua za kijeshi za Marekani katika Ghuba ya Uajemi
Aug 04, 2019 02:25Kuongezema mivutano katika eneo la Ghuba ya Uajemi kulikosababishwa na hatua za kichokozi na vitisho za Marekani na vile vile hatua ya Iran ya kuisimamisha meli ya mafuta ya Uingereza kwa kukiuka wazi wazi sheria za baharini kumezipelekea Washington na London kufanya kila linalowezekana ili kuimarisha uwepo wao wa kijeshi sambamba na kuanzisha muungano wa baharini eti kwa ajili ya kudhamini usalama wa meli huru katika eneo hilo la kistratejia.
-
Vikwazo dhidi ya Zarif; upinzani wa kimataifa dhidi ya Marekani
Aug 02, 2019 20:54Hatua ya Marekani kumuwekea vikwazo Muhammad Jawad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekabiliwa na upinzani mkali wa jamii ya kimataifa, hatua ya kisiasa ambayo imekosolewa hata ndani ya Marekani kwenyewe.
-
Malengo ya safari ya kiduru ya Jared Kushner katika eneo la Asia Magharibi
Aug 02, 2019 02:45Jared Kushner, mshauri mkuu wa Rais Donald Trump wa Marekani Jumatano iliyopita alianza safari ya kiduru katika eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati).
-
Ukosoaji wa Russia kwa utendaji wa Umoja wa Mataifa mkabala na jinai za magaidi nchini Syria
Aug 01, 2019 20:46Syria imekuwa ikikabiliwa na hali ya mchafukoge tangu mwakak 2011 na kisha ikatumbukia katika vita vya ndani baina ya serikali halali ya Rais Bashar al-Assad wa nchi hiyo na waungaji mkono wake kwa upande mmoja na makundi ya kigaidi yanayoungwa mkono na madola ya Magharibi na washirika wao wa Kiarabu kwa upande wa pili.
-
Rais Rouhani: Marekani imeshindwa na kufeli mbele ya taifa la Iran
Aug 01, 2019 08:02Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mwaka jana maadui wa taifa la Iran walidai kuwa wanaweza kuuondoa madarakana mfumo wa Kiislamu unaotawala Iran, kuvunja uhuru wake na kuweka hatamu za nchi hiyo katika mikono ya White House, lakini hawakujua kwamba taifa la Iran litashinda na kuzima mashinikizo ya adui.
-
Ujerumani yapinga kujiunga na muungano wa baharini wa Marekani katika Ghuba ya Ujemi
Jul 31, 2019 06:39Kudhihiri mivutano katika eneo la Ghuba ya Ujemi kutokana na kuongezeka uwepo wa kijeshi wa Marekani katika eneo hili lenye umuhimu wa kistratijia na vilevile kukamatwa meli ya Uingereza na wanajeshi wa Iran kutokana na kukiuka kwake wazi wazi sheria za usafiri wa baharini, kumezipelekea Washington na London kujaribu kubuni muungano wa baharini kwa madai ya kulinda usalama wa safari za meli katika eneo hilo.
-
Russia yawasilisha mpango wa usalama wa Ghuba ya Uajemi kwa Umoja wa Mataifa
Jul 30, 2019 06:24Uwepo wa kijeshi wa nchi za kigeni katika eneo la Ghuba ya Uajemi na taathira zake mbaya ambazo zimepelekea kuongezeka mivutano ya kisiasa na kijeshi katika eneo, umeipelekea Russia kuwasilisha mpango wa usalama wa eneo hili la kistratijia kwa Umoja wa Mataifa.
-
Hossein Amir-Abdollahian: Marekani chanzo cha ukosefu wa usalama na amani nchini Afghanistan
Jul 30, 2019 03:15Hossein Amir-Abdollahian, Msaidizi Maalumu wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amesema kuwa, siasa mbovu za Marekani ndio chimbuko la ukosefu wa usalama na amani nchini Afghanistan.
-
Ansarullah ya Yemen: Marekani na Umoja wa Mataifa zinachangia jinai za Saudi Arabia
Jul 30, 2019 02:46Harakati ya Ansarullah ya Yemen imetangaza kuwa, serikali ya Marekani na Umoja wa Mataifa zinabeba jukumu la jinai zinazofanywa na muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia.
-
Kujiuzulu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Taifa wa Marekani
Jul 30, 2019 02:17Tangu Donald Trump aliposhika hatamu za kuongoza Marekkani alianza kutekeleza sera ya kuwafukuza kazi na hata kuwalazimisha maafisa wa ikulu ya White House wajiengue wenyewe.