-
Kuendelea mashinikizo dhidi ya mbunge mwanamke Muislamu wa Kongresi ya Marekani
Mar 04, 2019 04:07Katika muendelezo wa mashinikizo dhidi ya Ilhan Omar, mbunge Muislamu wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, kwa mara nyingine, wafuasi na waungaji mkono wa Rais Donald Trump wa Marekani wamemtusi mbunge huyo kwa kubandika picha zinazomtambulisha yeye kama gaidi.
-
Bwabwaja mpya za Mike Pence dhidi ya Iran, kukaririwa tuhuma bandia
Mar 03, 2019 23:09Marekani katika kipindi cha uongozi wa Rais Donald Trump, imeonyesha wazi misimamo yake ya kudhoofisha na kujaribu kuundoa madarakani mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu nchini Iran.
-
Polisi wa Marekani waliomuua kwa risasi 20 kijana mweusi wafutiwa mashitaka
Mar 03, 2019 04:23Katika kile kinachoonekana ni mwendelezo wa ukiukaji wa haki za kiraia za msingi za Wamarekani wenye asili ya Afrika, Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali katika wilaya ya Sacramento jimboni California nchini Marekani imewaondolea mashitaka maafisa wa polisi waliommiminia risasi na kumuua kijana mweusi ambaye hakuwa amejizatiti kwa silaha yoyote mwaka jana.
-
Sanders: Trump ni kidhabi na rais hatari zaidi katika historia ya US
Mar 03, 2019 04:15Seneta Bernie Sanders ambaye amezindua rasmi azma yake ya kugombea urais katika uchaguzi wa 2020 nchini Marekani amesema Donald Trump ndiye rais hatari zaidi katika historia ya hivi karibuni ya Marekani na kwamba mwanasiasa huyo wa chama cha Republican amekubuhu katika kusema urongo.
-
Syria: Marekani na Uturuki zinajua mahali alipo kiongozi wa DAESH (ISIS), Abu Bakr al-Baghdadi
Mar 02, 2019 22:56Syria imesema, Marekani na Uturuki zina taarifa za mahali alipo kiongozi wa kundi la kigaidi la DAESH (ISIS) Ibrahim al-Samarrai, anayejulikana pia kama Abdu Bakr al-Baghdadi.
-
Mgombea Urais 2020 nchini Marekani: Washington ilikosea kujiondoa katika mapatano ya JCPOA
Mar 01, 2019 23:19Mwanachama wa Bunge la Seneti na mgombea urais katika uchaguzi wa 2020 nchini Marekani, Elizabeth Warren sambamba na kuyatetea mapatano ya nyuklia ya Iran maarufu kama JCPOA amesema kuwa, hatua ya Washington kujiondoa katika mapatano hayo haikuwa na maana.
-
Kufeli vibaya Trump katika kampeni ya kuipokonya silaha za nyuklia Korea Kaskazini
Mar 01, 2019 10:26Licha ya majigambo na makelele mengi ya kipropaganda ya Donald Trump na madai yake ya kupata mafanikio makubwa katika kampeni yake ya kuipokonya silaha za nyuklia Korea Kaskazini, lakini rais huyo wa Marekani mwenye majivuno mengi amefeli vibaya katika suala hilo.
-
Maelfu ya watoto wahajiri wanaozuiliwa nchini Marekani wanabakwa
Feb 27, 2019 04:37Wizara ya Afya ya Marekani imepokea malalamiko zaidi ya 4,500 yanayohusu kudhalilishwa kingono watoto wahajiri wanaozuiliwa nchini humo.
-
Tishio la kijeshi; kuendelea hatua zilizogonga mwamba za Marekani dhidi ya Venezuela
Feb 26, 2019 23:13Sambamba na kuongezeka harakati za kijeshi za Marekani dhidi ya Venezuela, Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo ameituhumu Washington kwamba, inafanya njama za kuzusha mgogoro kwa shabaha ya kuanzisha vita katika eneo la Amerika ya Latini.
-
Ansarullah: Watoto na wanawake wa Yemen wanauawa kwa silaha za Marekani
Feb 26, 2019 04:31Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema wanawake na watoto wa nchi hiyo maskini ya Kiarabu wanauawa kikatili kwa silaha zilizoundwa na Marekani na Wamagharibi katika hujuma zinazoongozwa na Saudi Arabia na waitifaki wake.