-
Trump akosolewa kwa kuirejesha Ansarullah katika 'orodha ya magaidi'
Jan 23, 2025 04:19Watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekosoa vikali hatua ya Rais wa Marekani, Donald Trump ya kuanzisha mchakato wa kuirejesha Harakati ya Ansarullah ya Yemen katika orodha ya Washington ya makundi ya 'kigaidi'.
-
Mashirika ya haki yaonya; Trump atarejesha marufuku dhidi ya Waislamu
Jan 23, 2025 04:07Mashirika ya kutetea haki za kiraia nchini Marekani yameonya kuwa, amri ya utendaji iliyosainiwa na Rais Donald Trump siku ya Jumatatu inaweka msingi wa kurejesha marufuku ya wasafiri kutoka nchi zenye Waislamu na Waarabu wengi kuingia Marekani.
-
WHO yasikitishwa na Marekani kujiondoa kwenye shirika hilo
Jan 21, 2025 23:19Shirika la Afya Duniani (WHO) limeelezea masikitiko yake kufuatia tangazo la Rais wa Marekani Donald Trump la kuiondoa nchi hiyo kwenye shirika hilo. WHO imesema inatumai serikali mpya ya Washington itaangalia upya uamuzi wake huo.
-
Trump aapa kuweka hadharani nyaraka za siri za mauaji ya kina Kennedy na Martin Luther King Jr.
Jan 20, 2025 23:04Rais mpya wa Marekani Donald Trump ameahidi kuweka hadharani nyaraka za serikali zilizoainishwa kuwa za siri zaidi, zinazohusiana na mauaji ya Rais John F. Kennedy, Seneta Robert F. Kennedy, na mwanaharakati wa haki za kiraia Martin Luther King Jr.
-
Mtandao wa Salon: Marekani na Israel Zinaficha Ukweli Kuhusu Vita vya Gaza
Jan 20, 2025 04:00Mwandishi wa habari mashuhuri wa Marekani ameeleza mbinu zinazotumiwa na Marekani na utawala ghasibu wa Israel kuficha jinai za Wazayuni katika vita vya Gaza.
-
Wakuu wa Amerika Kusini: Uamuzi wa Trump wa kuwafukuza wahamiaji ni ukiukaji wa haki za binadamu
Jan 19, 2025 08:02Katika kipindi cha kukaribia kuanza awamu nyingine ya utawala wa Donald Trump kama Rais wa Marekani, wawakilishi na maafisa wa nchi mbalimbali za Amerika Kusini, katika tamko lao, wamebainisha wasiwasi wao kuhusu utekelezaji wa sera ya kufukuzwa wahamiaji kutoka nchi tofauti.
-
Canada: Tuko tayari kujibu vitisho vya ushuru vya Trump
Jan 18, 2025 07:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada amesema kuwa nchi hiyo imejiandaa kujibu hatua yoyote ya Washington ya kuiwekea Canada ushuru mpya. Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada ameeleza haya siku chache kabla Rais mteule wa Marekani, Donald Trump hajaanza kazi rasmi katika Ikulu ya White House.
-
Sullivan: Enzi ya ukuu wa Marekani imekwisha
Jan 15, 2025 23:06Mshauri wa Usalama wa Kitaifa wa Ikulu ya Rais wa Marekani, White House, amekiri kwamba: Zama za Marekani kuwa juu zaidi ya nchi nyingine zimekwisha na kuyoyoma.
-
TV ya Marekani yaonyesha mabaki ya silaha za nchi hiyo Ghaza zinazotumika katika mauaji ya kimbari
Jan 15, 2025 08:07Kanda za video zilizorushwa hewani na chaneli kubwa ya televisheni ya Marekani ya CBS zimefichua kuwepo kwa silaha nyingi ambazo serikali ya Washington imeupatia utawala wa Kizayuni wa Israel uzitumie katika mauaji ya kimbari ya Wapalestina unayofanya katika Ukanda wa Ghaza, suala ambalo limekabiliwa na malalamiko na ukosoaji mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.
-
WHO yasema hali ya Mpox nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ingali inatisha
Jan 14, 2025 23:13Shirika la Afya Duniani WHO limesema, ijapokuwa mwenendo wa sasa wa homa ya nyani au Mpox duniani inaonekana kutulia, lakini hali si shwari nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.