-
Papa Francis akosoa mpango wa Trump wa Muamala wa Karne
Feb 24, 2020 01:10Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, kwa njia isiyo ya moja kwa moja amekosoa mpango wa Rais Donald Trump wa Muamala wa Karne ambapo ameonya kuwa, mipango ya namna hiyo inayoegemea upande mmoja haiwezi kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Palestina na Israel.
-
Wapalestina kadhaa wauawa shahidi na wanajeshi wa Israel Ukanda wa Gaza
Feb 23, 2020 09:58Askari wa jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel wamewapiga risasi na kuwaua shahidi Wapalestina wawili katika uzio unaotenganisha Ukanda wa Gaza na ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
Umoja wa Ulaya: Tunaunga mkono kuundwa nchi huru ya Palestina
Feb 22, 2020 09:10Josep Borrell, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesisitiza kuwa, umoja huo unaunga mkono juhudi zinazofanyika kwa ajili ya kuundwa nchi huru ya Palestina.
-
Seneti ya Pakistan yapasisha azimio dhidi ya njama ya Trump ya "Muamala wa Karne"
Feb 20, 2020 04:45Baraza la Seneti la Pakistan limepasisha kwa sauti moja azimio linalopinga mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu Palestina uliopewa jina la "Muamala wa Karne" likisema kuwa unawataka Wapalestina wasalimu amri kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Askofu wa Kanisa Katoliki Lebanon: Mpango wa Muamala wa Karne ni namna fulani ya kutangaza vita
Feb 19, 2020 08:11Kiongozi wa Kanisa Katoliki kusini mwa Lebanon amesema kuwa, mpango wa kibaguzi wa Muamala wa Karne unakinzana wazi kabisa na amani na kuishi pamoja na kimsingi ni namna fulani ya kutangaza vita.
-
Utawala wa Kizayuni wajiepusha kuingia tena vitani na wanamuqawama wa Palestina
Feb 18, 2020 10:18Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni amesema kuwa utawala huo umeamua kujiepusha na kujiingiza vitani kwa mara nyingine tena na wanamuqawama wa Palestina.
-
Ujumbe wa jumuiya za Mayahudi watembelea Saudia kwa siri na kufanya mazungumzo katika kasri la Mfalme Salman
Feb 15, 2020 23:20Kanali ya Kwanza ya televisheni ya Israel imetangaza kuwa ujumbe uliojumuisha viongozi wa jumuiya za Kiyahudi za Marekani ulitembelea Saudi Arabia siku za hivi karibuni na kupokewa katika kasri la Mfalme Salman bin Abdul Azizi Aal Saud mjini Riyadh.
-
Saudia yaanzisha wimbi jipya la kuwatia mbaroni Wapalestina
Feb 14, 2020 04:02Utawala wa Aal-Saud umeanzisha wimbi jipya la kuwakamata na kuwazuilia raia wa Palestina wanaoishi Saudi Arabia kwa madai ya kuiunga mkono Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas).
-
Mousavi: Iran itatoa jibu kali kwa hatua yoyote ya kijinga ya Israel
Feb 13, 2020 01:06Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: "Iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utatekeleza uvamizi au hatua yoyote ya kijinga dhidi ya maslahi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Syria na katika eneo, basi utawala huo utapokea jibu kali ambalo litakuwa la majuto."
-
Rais Abbas kwa Baraza la Usalama: Muamala wa Karne unakiuka maazimio ya UN
Feb 12, 2020 04:10Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa, mbali na mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani uliopewa jina la Muamala wa Karne kukanyaga maazimio ya umoja huo, pia unakiuka mamlaka na uhuru wa kujitawala Palestina.