-
Sababu za kuongezeka hukumu za kifo nchini Saudi Arabia baada ya Bin Salman kuingia madarakani
Feb 02, 2023 23:36Shirika la Haki za Binadamu la Ulaya-Saudia, limetangaza katika ripoti ya karibuni kwamba hukumu za kifo au unyongaji wakati wa utawala wa mrithi wa kiti cha ufalme Mohammed bin Salman nchini Saudi Arabia zinaongezeka karibu mara mbili kila mwaka.
-
Taasisi za haki za binadamu zaidi ya 170 zataka kuhitimishwa maafa ya binadamu Yemen
Jan 26, 2023 05:13Mashirika na taasisi za haki za binadamu za kimataifa zaidi ya 170 zimetaka kuhitimishwa maafa ya binadamu huko Yemen na mzingiro dhidi ya nchi hiyo.
-
Utawala wa Saudia wamhukumu kifo profesa wa chuo kikuu kwa kuiunga mkono Ikhwanul Muslimin
Jan 15, 2023 23:41Utawala wa Saudi Arabia umemhukumu kifo Profesa maarufu wa Chuo Kikuu kwa kutumia mitandao ya kijamii ya Twitter na WhatsApp kuliunga mkono kundi la Ikhwanul Muslimin na kusambaza habari zinazodaiwa kuwa za uhasama dhidi ya ufalme huo wa Aal Saud unaowakandamiza wapinzani na wanaharakati wa mageuzi nchini humo.
-
Biashara ya bidhaa za Iran yazidi kunawiri nchini Saudi Arabia
Jan 09, 2023 22:59Usafirishaji nje wa bidhaa za Iran kuelekea nchini Saudi Arabia umestawi hivi sasa baada ya kuanza mazungumzo baina ya nchi hizi mbili za Waislamu. Hayo yametokea baada ya biashara baina ya pande mbili kuzorota kwa miaka kadhaa.
-
Shirika la kutetea haki za binadamu laonya, Saudia inawanyonga wafungwa kwa sababu za kiitikadi
Dec 28, 2022 04:32Shirika la kutetea haki za binadamu la Sanad limetangaza kuwa limepokea taarifa zinazoonyesha nia ya Saudi Arabia ya kutekeleza hukumu za kifo kwa idadi ya wafungwa wa itikadi na wanajeshi.
-
Mmoja wa wakurugenzi wa Twitter ahukumiwa kifungo kwa kuifanyia ujasusi Saudi Arabia
Dec 15, 2022 07:12Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Marekani imepelekea kuhukumiwa mmoja wa wakurugenzi wa zamani wa mtandao wa kijamii wa Twitter kifungo cha miaka mitatu na nusu jela kwa tuhuma za kufanya ujasusi kwa manufaa ya Saudi Arabia.
-
Mbunge wa Kizayuni afichua: 2023 Saudia na Israel zitasaini mkataba wa kuanzisha uhusiano rasmi
Dec 13, 2022 22:56Mbunge wa chama cha Likud katika Bunge la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel amesema, kwa kuzingatia mazungumzo yaliyofanyika, inatarajiwa kuwa makubaliano ya kuanzishwa uhusiano wa kawaida kati ya utawala huo na Saudi Arabia yatasainiwa mwaka ujao wa 2023.
-
Saudia yakosolewa kwa kuzima sauti ya adhana kwa ajili ya hafla za ufuska
Dec 07, 2022 22:51Licha ya ukandamizaji wa kimfumo wa utawala wa Saudia dhidi ya wale wanaokosoa mwelekeo wa kisiasa na kijamii wa utawala huo unaolazimishwa kwa watu kwa mabavu, sauti zimeanza kupazwa nchini humo dhidi ya hafla na sherehe za ufuska na ufisadi zinazoandaliwa na kile kinachoitwa Mamlaka Kuu ya Burudani katika Ufalme huo.
-
Umoja wa Mataifa wakosoa vikali hukumu za kukatwa watu vichwa Saudi Arabia
Nov 22, 2022 23:09Mmoja wa wasemaji wanaohusika na haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa ameelezea masikitiko yake kuhusu utekelezwaji wa hukumu za vifo kwa kukata watu vichwa nchini Saudi Arabia.
-
Bin Salman ajibiwa: Kuvunjiwa heshima Haram Mbili Takatifu haliwi tena suala la ndani la Saudia
Nov 08, 2022 04:08Wanaharakati wa mitandao ya kijamii wamemjibu Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia aliyedai kwamba hakuna mtu yeyote mwenye haki ya kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo kwa kumueleza kuwa kutusi na kuvunjia heshima nchi ambayo ndani yake kuna Haram mbili za Makka na Madina haliwi suala la ndani la Saudia.