-
Al-Burhan: Hakutakuwa na suluhu Sudan mpaka RSF iondoke kwenye maeneo yote inayoyakalia
Feb 21, 2026 02:23Mkuu wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, amesema hakutakuwa na usitishaji mapigano mpaka pale Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) vitakapojiondoa kwenye kile alichokieleza kuwa ni maeneo vinayoyakalia na kujikusanya upya katika maeneo yaliyotengwa.
-
Wachunguzi wa UN: Yumkini mauaji ya halaiki yamefanyika El-Fasher
Feb 20, 2026 03:27Ujumbe wa kutafuta ukweli wa Umoja wa Mataifa umesema ukatili uliofanywa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF wakati wa kuutwaa mji wa El-Fasher huko Darfur Magharibi nchini Sudan mwezi Oktoba mwaka jana, una "alama za mauaji ya kimbari" dhidi ya jamii za Zaghawa na Fur.
-
Nchi 24 zaonya kuhusu janga la watu nchini Sudan; UN yasema ina wasiwasi mkubwa
Feb 19, 2026 03:03Nchi 24 za Magharibi zimeelezea wasiwasi wao kuhusu mauaji yanayoendelea kufanywa dhidi ya raia, uharibifu wa miundombinu na mashambulizi dhidi ya taasisi za misaada ya kibinadamu nchini Sudan, zikitoa wito kwa jeshi la Sudan na wapiganaji wa kundi la waasi la Rapid Support Forces kusitisha mapigano.
-
Watu 3 wameuawa na 7 kujeruhiwa katika shambulio la droni la RSF hospitalini katika jimbo la Sennar, Sudan
Feb 17, 2026 02:27Mashambulizi wa ndege zisizo na rubani (droni) ya wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF)yameuwa watu watatu na kuwajeruhi wengine saba katika Hospitali ya Al-Mazmoum katika jimbo la Sennar kusini mashariki mwa Sudan.
-
Takriban watu 21 wameaga dunia baada ya boti kuzama katika Mto Nile, Sudan
Feb 13, 2026 07:20Takriban watu 21 wamekufa maji wakati boti iliyokuwa ikiwasafirisha ilipozama katika Mto Nile kaskazini mwa Sudan.
-
Mashambulizi ya droni ya wanamgambo wa RSF yaua watu 2 na kujeruhi 4 Kordofan, Sudan
Feb 13, 2026 07:20Mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) za wanamgambo wa kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) yameuwa raia wawili na kujeruhi wanne katika jimbo la Kordofan Kusini. Haya yamebainishwa jana Mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
Sudan yataka irejeshewe uanachama katika Umoja wa Afrika
Feb 13, 2026 02:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Muhi al-Din Salem Ahmed amekariri wito wake kwa Umoja wa Afrika, akiitaka AU kufuta hatua yake ya kuisimamishia uanachama nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika katika umoja huo.
-
Shambulio la droni la RSF laua watu 24 wakiwemo watoto 8 Kordofan Kaskazini, Sudan
Feb 08, 2026 02:29Shambulio la ndege zisizo na rubani la Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF lililolenga gari lililobeba familia za raia wa Sudan waliolazimika kuyahama makazi yao limeua watu wasiopungua 24, wakiwemo watoto wanane. Hayo ni kwa mujibu wa shirika la mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
Watu 22 wauawa katika shambulio la RSF katika hospitali ya kijeshi Kordofan Kusini
Feb 06, 2026 02:29Watu wasiopungua 22 wakiwemo wahudumu 4 wa sekta ya afya wameuawa na wengine wawane kujeruhiwa baada ya wanangambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) jana kuishambulia hospitali ya jeshi ya al Kuweik katika jimbo la Kordofan Kusini nchini Sudan.
-
Mashambulizi ya droni yaua watu 15 Kadugli, kusini mwa Sudan
Feb 04, 2026 10:22Raia wasiopungua 15, wakiwemo watoto saba, wameuawa katika mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika mji wa Kadugli kusini mwa Sudan. Hayo yamesemwa na kundi la kujitolea la wenyeji na mashuhuda wa hujuma hiyo ambao wameeleza kuwa, mashambulizi hayo yamejiri saa chache baada ya jeshi la Sudan kutangaza kuvunja mzingiro wa miaka mingi dhidi ya mji wa Kadugli.