-
Khartoum yatoa ushahidi dhidi ya UAE na kuikosoa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai
Jul 18, 2026 09:07Waziri wa Sheria wa Sudan, Abdullah Darf, amewasilisha kifurushi cha njia za kisheria "zisizo za kawaida" ambazo serikali ya Khartoum inakusudia kuchukua ili kufungua mashtaka dhidi ya serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF), akisisitiza kwamba Khartoum ina "ushahidi wa kutosha na data kamili" kuhusu "ushiriki wa Abu Dhabi katika vita na uhalifu uliofanywa na pande hizo mbili dhidi ya watu wa Sudan."
-
Umoja wa Mataifa waonya dhidi ya kutumia vibaya rasilimali za Sudan kufadhili vita
Jul 16, 2026 03:04Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba makundi yanayopigana nchini Sudan yanafaidika kutokana na udhibiti wa rasilimali za nchi hiyo, wakati uchumi wa vita ukichangia katika kuendeleza mzozo huo.
-
Jeshi la Sudan lakomboa eneo la Fashfoun katika jimbo la Blue Nile baada ya mapigano na waasi
Jul 14, 2026 11:03Jeshi la Sudan limesema mapema Jumanne kuwa limekomboa eneo la Fashfoun katika jimbo la Blue Nile baada ya mapigano na waasi wa makundi ya RSF na SPLM-N.
-
Shirika la haki za binadamu: RSF inawashikilia raia 6,000 katika magereza ya El Fasher
Jul 13, 2026 08:15Ripoti iliyoandaliwa na Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu nchini Sudan imeonyesha kuwa watu 6,000 wanashikiliwa na wapiganaji wa kundi la waasi la Rapid Support Forces (RSF) katika magereza huko El Fasher, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, magharibi mwa nchi, na pia imerekodi ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na kundi hilo dhidi ya raia.
-
Serikali ya Sudan na UNICEF zaonya kuhusu kuzorota hali ya kiafya katika maeneo yenye migogoro
Jul 12, 2026 10:46Serikali ya Sudan na Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF) zimeonya kuhusu mgogoro mbaya wa utapiamlo miongoni mwa watoto nchini Sudan, huku vita na mapigano ya ndani yakiendelea kwa mwaka wa nne sasa.
-
Alkhamisi, tarehe 9 Julai, 2026
Jul 09, 2026 03:17Leo ni Alkhamisi tarehe 24 Mfunguo Nne Muharram 1448 Hijria inayosadifiana na tarehe 9 Julai 2026.
-
Shambulio la droni la RSF lauwa raia 10 waliokuwa wakielekea harusini katikati mwa Sudan
Jul 08, 2026 12:20Mtandao wa Madaktari wa Sudan leo umeripoti kuwa shambulio la ndege zisizo na rubani lililofanywa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) limeua raia 10, wakiwemo wanawake watano kutoka familia moja, katikati mwa Sudan walipokuwa wakieleke harusini.
-
IOM : Mashambulizi ya RSF yanaweza kuifanya El Obeid nchini Sudan kuwa 'El Fasher nyingine'
Jul 06, 2026 02:48Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limetahdharisha kuwa mji wa El-Obeid nchini Sudan, ambao ni makao makuu ya Jimbo la Kordofan Kaskazini, unaweza kukumbwa na hatima sawa na ile iliyoupata mji wa El Fasher katika jimbo jirani la Darfur Kaskazini iwapo mashambulizi yanayofanywa na wanamgambo wa kikosi cha Msaada wa Haraka, Rapid Support Forces (RSF) yataendelea.
-
Raia 11 wauawa katika shambulio la droni sokoni Kordofan Kaskazini nchini Sudan
Jun 07, 2026 11:08Shambulio la ndege zisizo na rubani sokoni katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan limeua takriban raia 11 na kujeruhi makumi ya wengine.
-
Jeshi la Sudan lazuia shambulio la RSF huko Blue Nile
Jun 04, 2026 11:19Jeshi la Sudan limetangaza kuwa limezima shambulio la Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kwenye eneo la kimkakati la Al-Baraka nje kidogo ya mji wa Kurmuk katika Jimbo la Blue Nile, kusini mashariki mwa nchi hiyo.