-
UN: Vita nchini Sudan vimepelekea watu zaidi ya milioni tatu kuwa wakimbizi
Jul 13, 2023 04:28Umoja wa Mataifa umeeleza kuwa vita vya karibu miezi mitatu huko Sudan vimepelekea watu zaidi ya milioni tatu kuwa wakimbizi na kutoa wito kwa pande zinazopigana kuwajibika.
-
Sudan yapinga majeshi ya kigeni kupelekwa nchini humo
Jul 12, 2023 23:28Sudan imepinga kutumwa wanajeshi wa kigeni nchini humo na kutangaza kuwa itawachukulia wanajeshi hao kuwa ni sawa na askari vamizi.
-
Indhari ya Katibu Mkuu wa UN ya kufikia Sudan kwenye ukingo wa vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe
Jul 11, 2023 08:00Mapigano nchini Sudan yanaendelea kupamba moto, na juhudi zilizofanywa hadi sasa za kuleta suluhu na kurejesha amani na utulivu katika nchi hiyo sio tu hazijafanikiwa, lakini pande mbili zinazopigana zimeshadidisha pia mashambulizi yao. Kutokana na hali hiyo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametahadharisha kuwa, Sudan sasa imeshafika kwenye ukingo wa vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe.
-
Jeshi la Sudan lakataa kushiriki mkutano wa IGAD nchini Ethiopia
Jul 11, 2023 04:05Jeshi la Sudan limekataa kushiriki mkutano wa ngazi ya juu wa kuzindua mchakato wa amani wa nchi hiyo uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia; huku mapigano yakishtadi katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la anga Sudan lililoua watu 22 Omdurman
Jul 10, 2023 03:53Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani shambulizi la anga lililotokea Omdurman nchini Sudan, ambalo limeripotiwa kuua takriban watu 22.
-
Iran na Sudan kufufua uhusiano wao wa kidiplomasia karibuni
Jul 06, 2023 23:38Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekutana na kufanya mazungumzo na mwenzake wa Sudan kwa mara ya kwanza baada ya miaka saba, ambapo wamekubaliana kufufua uhusiano wa kidiplomasia wa nchio mbili hizi karibuni hivi.
-
Baraza la Usalama latakiwa kushughulia jinai dhidi ya raia katika mapigano ya Sudan
Jun 28, 2023 23:22Asasi na jumuiya 41 zenye mfungamano na wanawake Afrika, zimelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufuatilia na kushughulikia jinai dhidi ya raia nchini Sudan zinazofanywa na pande mbili hasimu katika vita vyao.
-
Kikosi cha RSF chasitisha vita Sudan kwa saa 48 kwa ajili ya Iddul Adh'ha
Jun 27, 2023 03:26Kikosi cha Radiamali ya Haraka cha Sudan (RSF) kimetangaza habari ya usitishaji vita wa upande mmoja wa saa 48 kuanzia leo Jumanne, kwa ajili ya maadhimisho ya Sikukuu ya Idul Adh'ha.
-
Pande hasimu Sudan zatakiwa kuweka silaha chini kuelekea Iddul Adh'ha
Jun 23, 2023 06:50Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imetoa mwito kwa vikosi hasimu vinavyopigana nchini Sudan kusitisha mapigano, wakati huu ambapo taifa hilo kama mataifa mengine ya Waislamu, linakaribia kuadhimisha Sikukuu ya Iddul Adh'ha (Iddul Hajj).
-
Wafadhili waahidi kutoa msaada wa dola bilioni 1.5 kwa ajili ya Sudan
Jun 20, 2023 04:35Wafadhili wameahidi katika Mkutano wa Geneva wa Kukabiliana na Mgogoro wa Sudan, kutoa msaada wa kibinadamu wa takriban dola bilioni 1.5, wakati huu ambapo hali ya utulivu imetanda kwa kiasi fulani nchini Sudan kwa siku ya pili kutokana na makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa baina ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF).