-
WFP: Familia nchini Sudan zinapitia kipindi kigumu kufuatia mizozo ya kikatili, njaa na uhaba wa fedha
Jan 15, 2026 23:23Familia nchini Sudan zinasukumwa ukingoni huku "migogoro ya kikatili" na njaa vikiendelea. Mpango wa Chakula Duniani (WFP) pia umetahadharisha kuwa oparesheni zake za kibinadamu za kunusuru maisha ya wananchi wa Sudan zinasusua kufuatia uhaba mkubwa wa fedha.
-
Misri: Umoja wa Sudan ni mstari mwekundu kwetu, hatutasita kuchukua kila hatua kuulinda
Jan 15, 2026 22:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty amesema, nchi yake itachukua hatua zote zinazohitajika ili kuhifadhi umoja wa ardhi ya Sudan, wakati nchi hiyo jirani inakaribia kuingia mwaka wake wa nne wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyohusisha vikosi vya jeshi SAF na vile vya usaidizi wa haraka, RSF.
-
Madaktari Sudan watahadharisha kuhusu maafa tarajiwa ya kibinadamu huko Kordofan Kusini
Jan 04, 2026 03:35Kundi la madakatri wa Sudan limetahadharisha kuhusu maafa tarajiwa ya kiafya na kibinadamu katika mji wa Dalang unaopatikana katika jimbo la Kordofan Kusini. Kundi hilo limesema kuwa mji wa Dalang unaendelea kuzingirwa huku ukikabiliwa na mashambulizi makali ya wanagambo wa RFS.
-
UN yakumbana na hali mbaya El Fasher katika ziara yake ya kwanza tangu mji huo udhibitiwe na RSF
Jan 01, 2026 07:43Umoja wa Mataifa umeripoti kuwa mji wa El- Fasher huko Darfur Magharibi nchini Sudan unapitia hali ya kutisha kwa binadamu.
-
Jeshi la Sudan lakomboa miji miwili ya Kordofan Kaskazini kutoka mikononi mwa RSF
Jan 01, 2026 02:16Jeshi la Sudan SAF limetangaza kuwa siku ya Jumatano lilirejesha udhibiti wa miji ya Kazgeil na Riyadh iliyoko kwenye jimbo la Kordofan Kaskazini baada ya mapigano na kundi la RSF.
-
Alkhamisi tarehe Mosi Januari, mwaka 2026
Dec 31, 2025 23:15Leo ni Alkhamisi tarehe 11 Rajab 1447 Hijria sawa na tarehe Mosi Januari mwaka 2026.
-
Wanawake na watoto ni kati watu zaidi ya 200 waliouawa katika mauaji mapya ya kikabila huko Darfur
Dec 28, 2025 07:09Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeripoti kuwa watu zaidi ya 200, wakiwemo wanawake na watoto wameuawa katika mashambulizi ya kikabila yaliyofanywa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) huko Darfur nchini Sudan.
-
Kuzidi kuwa tata vita vya Sudan; indhari ya Umoja wa Mataifa kuhusu kupanuka wigo wake
Dec 23, 2025 08:24Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa sanjari na kusisitiza umuhimu wa kusitisha vita nchini Sudan, ameonya kuhusu utambulisho wake tata na athari zake zinazopanuka kwa nchi jirani na eneo kwa ujumla.
-
Wanamgambo wa RSF wamewaachia huru wafanyakazi 9 wa sekta ya afya huko Darfur
Dec 20, 2025 10:33Mtandao wa Madktari nchini Sudan umeripoti kuwa wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) umewaachia huru wafanyakazi 9 wa sekta ya afya waliokuwa wakishikiliwa katika magareza na kikosi hicho huko Nyala makao makuu ya jimbo la Darfur Kusini. Hata hivyo kikosi cha RSF bado kinawashikilia wafanyakazi wengine wa afya 73.
-
Mashambulizi ya RSF yaua raia 16 eneo la Kordofan, Sudan
Dec 19, 2025 23:07Takriban watu 16 wameuawa katika shambulio la mizinga la waasi wa RSF lililolenga mji uliozingirwa katika eneo la Kordofan nchini Sudan, huku vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo vikiingia katika awamu hasasi kwenye mwaka wake wa tatu.