-
Makumi ya maiti zapatikana kwenye mto ulioko mpakani mwa eneo la Ethiopia la Tigray na Sudan
Aug 03, 2021 07:45Maiti zisizopungua 30 zilizosombwa na maji zimepatikana kwenye kingo za mto unaotenganisha Sudan na eneo la kaskazini mwa Ethiopia la Tigray. Hayo ni kwa mujibu wa wakimbizi wawili wa Ethiopia na mashuhuda wanne raia wa Sudan waliookota maiti hizo.
-
Sudan yasema Bwawa la an-Nahdha linahatarisha viwanda vyake vya kuzalisha umeme
Aug 02, 2021 06:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan amedai kwamba serikali ya nchi hiyo kutokuwa na habari kuhusu mwenendo wa kujazwa maji Bwawa la an-Nahdha katika nchi jirani ya Ethiopia ni tishio kwa viwanda vyake vya kuzalisha umeme.
-
Waethiopia elfu 3 wakimbilia Sudan wakihepa vita katika eneo la Tigray
Jul 28, 2021 22:02Vyombo vya habari vimetangaza kuwa, wakimbizi wa Kiethiopia zaidi ya elfu tatu wamewasili Sudan katika kipindi cha siku moja tu kufuatia mapigano yanayoendelea huko Tigray kaskazini mwa Ethiopia.
-
Jeshi la Ethiopia lasema liko tayari kulinda Bwawa la Renaissance
Jul 23, 2021 23:25Meja Jenerali Yalma Merdasa, Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Ethiopia, amesema kwamba kikosi hicho hakijatoa jicho lake kwenye Bwawa la Renaissance hata kwa dakika moja, na kwamba kiko tayari kulinda usalama wa anga wa nchi hiyo.
-
Sudan yaionya Ethiopia kuhusu Bwawa la al Nahdha
Jul 22, 2021 06:21Waziri Mkuu wa Sudan ametoa onyo kwa serikali ya Ethioia isichukue uamuzi wowote wa upande mmoja kuhusu mgogoro wa Bwawa la al Nahdha.
-
Zoezi la kumimina maji kwa awamu ya pili katika Bwawa la al Nahdha lamalizika
Jul 19, 2021 21:51Licha ya kuweko maonyo na vitisho vikali vya Sudan na Misri, lakini duru moja ya masuala ya umwagiliaji maji nchini Ethiopia imesema kuwa, zoezi la kumimina maji kwa awamu ya pili katika Bwawa la al Nahdha limekamilika.
-
Indhari kuhusu hatari ya kujiri vita vya ndani huko Sudan
Jul 03, 2021 22:38Chama kimoja cha kisiasa nchini Sudan kimetahadharisha kuhusu mapigano yanayoendelea kati ya makundi ya wanamgambo na kuwepo hatari ya kujiri vita vya ndani nchini humo.
-
Sudan katika lindi la maandamano mapya ya wananchi
Jul 01, 2021 21:58Mgogoro wa kisiasa na kuchumi unaendele kuisumbua Sudan licha ya kupita miaka miwili sasa tangu baada ya harakati ya wananchi iliyopelekea kuondolewa madarakani utawala wa miaka 30 wa Omar al Bashir na kuundwa serikali mpya nchini humo.
-
Ombi la Misri na Sudan kwa Baraza la Usalama; mgogoro wa Bwawa la An Nahda
Jun 28, 2021 05:56Huku awamu ya pili ya kujazwa maji katika Bwawa la An Nahda (Grand Renaissance Dam-GERD-) la Ethiopia katika Mto Nile ikikaribia, Misri na Sudan, nchi mbili ambazo zinapinga ujenzi wa bwawa hilo, zimetaka ujazwaji maji huo usitishwe kwa muda. Nchi hizo mbili zimetaka Ethiopia izipatie dhamana kuwa haki zao zitalindwa, jambo ambalo limeibua taharuki mpya baina ya nchi hizo tatu.
-
Sudan yakubali kwa masharti makubaliano ya muda ya Bwawa la Renaissance
Jun 28, 2021 04:57Waziri wa Mambo ya nje wa Sudan Mariam Al-Sadiq Al-Mahdi amesema kuwa nchi yake imepokea pendekezo kutoka kwa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo la makubaliano ya muda ya kujazwa maji Bwawa la Renaissance yanayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na Marekani.