-
Kuongezeka upinzani dhidi ya Umoja wa Ulaya katika nchi za bara hilo
Nov 27, 2023 22:54Baada ya ushindi wa Geert Wilders, mgombea wa mrengo wa kulia wa Uholanzi katika uchaguzi wa nchi hiyo na kupendekeza kwake suala la Uholanzi kujiondoa katika Umoja wa Ulaya, Marine Le Pen, kiongozi wa chama cha mrengo wa kulia cha National Rally cha Ufaransa, pia amesisitiza haya ya Ufaransa kujiondoa katika Umoja wa Ulaya akisema: 'Hatupingi Ulaya, tunapinga Umoja wa Ulaya na ni kwa sababu tunaipenda Ulaya, ndio maana tunaupinga Umoja huo.'
-
Ushindi wa mrengo wa kulia wenye misimamo mikali katika uchaguzi wa Uholanzi; kengele ya hatari kwa Ulaya
Nov 23, 2023 06:59Uchaguzi mkuu wa Uholanzi ulifanyika Jumatano, Novemba 22 nchini humo ili kubaini nani ataongoza serikali ijayo ambayo inapaswa kuchukua mamlaka nchini baada ya kuondoka Mark Rutte, ambaye amekuwa waziri mkuu kwa miaka 13.
-
EU yazidi kuandamwa na lawama kwa msimamo wake wa upendeleo katika kadhia ya Gaza
Nov 22, 2023 00:01Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ametahadharisha kuwa umoja huo unakabiliwa na chuki zinazoongezeka katika Ulimwengu wa Kiislamu na nje yake kutokana na shutuma za kuegemea upande wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kuwa na misimamo ya undumilakuwili kuhusiana na Vita vya Gaza.
-
HAMAS: Borrell anapindua ukweli wa mambo kuhusu Ghaza
Nov 13, 2023 10:14Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema kuwa, matamshi ya mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya dhidi ya makundi ya muqawama ni kupindua uhakika wa mambo na ni kujaribu kufunika jinai za utawala wa Kizayuni.
-
EU yapata hasara ya dola trilioni 1.5 kwa vikwazo dhidi ya Russia
Nov 03, 2023 08:56Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya zimepoteza takriban dola trilioni 1.5 kutokana na vikwazo vya Wamagharibi dhidi ya Moscow.
-
EU: Mashambulio ya utawala wa Kizayuni Ukanda wa Ghaza yanakanyaga sheria za kimataifa
Oct 29, 2023 02:27Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni kwenye maeneo ya makazi ya watu, vituo vya matibabu na skuli za Ghaza yanakanyaga sheria za kimataifa na utu na ubinadamu.
-
Jitihada za Magharibi za kuzuia kuakisiwa habari za Wapalestina katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari
Oct 14, 2023 22:53Baada ya kuanza oparesheni kwa jina la "Kimbunga cha Al Aqsa" iliyotekelezwa na Hamas na makundi mengine ya mapambano ya Palestina; serikali na vyombo vya habari vya Magharibi kwa upande mmoja vimeanzisha propaganda kubwa ili kuzuia kuakisiwa habari na matukio yanayojiri huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu huku vikichapisha na kutoa habari za uwongo ili kuonyesha taswira isiyo ya kibinadamu kuhusu wanamapambano wa Palestina.
-
EU: Israel inakanyaga sheria za kimataifa kwa kuiwekea mzingiro Gaza
Oct 11, 2023 08:38Umoja wa Ulaya umesema kuwa utawala wa Israel umekiuka sheria za kimataifa kwa kuuweka Ukanda wa Gaza chini ya mzingiro.
-
Kuendelea hitilafu katika Umoja wa Ulaya kuhusu wahamiaji
Oct 07, 2023 22:57Hitilafu kuhusu kadhia ya wahamiaji miongoni mwa nchi za Umoja wa Ulaya zingali zinaendelea licha ya makubaliano ya hivi karibuni kuhusu suala hilo.
-
Tunisia yakataa msaada wa kifedha wa Umoja wa Ulaya
Oct 04, 2023 23:46Rais Kais Saied wa Tunisia amekataa kupokea msaada wa kifedha wa Umoja wa Ulaya (EU) uliokusudia kupiga jeki bajeti ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika, sanjari na kuisaidia kukabiliana na mgogoro wa wakimbizi.