-
Iran yalaani urejeshaji vikwazo vya UN vilivyokwisha muda wake uliofanywa na Marekani na Ulaya
Sep 30, 2025 07:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi ameikosoa Marekani na mataifa matatu ya Ulaya kwa kujaribu kutumia utaratibu wa 'snapback' wa makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015 ili kurejesha tena vikwazo vilivyokwisha muda wake vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Lavrov: NATO na Umoja wa Ulaya zinapigana vita dhidi ya Russia Ukraine
Sep 27, 2025 02:15Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov amesema, mgogoro wa Ukraine ulipangwa na nchi za Magharibi kwa sura ya vita dhidi ya Russia vinavyopiganwa na Kiev.
-
Rais wa Baraza la EU: Lengo hasa la Israel ni kuufanya uundwaji wa nchi ya Palestina usiwezekane
Sep 23, 2025 02:57Rais wa Baraza la Ulaya Antonio Costa amesema hatua za kijeshi zinazochukuliwa na Israel huko Ghaza si suala tena la kujilinda na zinaonekana kuwa na lengo la kuufanya uundaji wa nchi ya Palestina hapo baadaye usiwezekane.
-
UN, AU na EU zaahidi kushirikiana kwa ajili ya amani na maendeleo barani Afrika
Sep 23, 2025 02:57Viongozi wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika AU na Umoja wa Ulaya EU, wametilia mkazo tena dhamira yao ya kuendeleza amani na maendeleo endelevu barani Afrika, kwa kuahidi ushirikiano wa kina zaidi ili kukomesha migogoro, kuimarisha mnepo na kukabiliana na changamoto za kimataifa kuanzia madeni hadi mabadiliko ya tabianchi.
-
Financial Times: EU inapanga kuzitumia yuro bilioni 170 fedha za Russia inazozishikilia
Sep 18, 2025 10:11Gazeti la Financial Times limeripoti kuwa Umoja wa Ulaya (EU) umeamua kutekeleza mpango wa kuzitumia yuro bilioni 170 milki za Russia inazozishikilia kurudisha "mikopo ya fidia" kwa Ukraine.
-
Kwa nini maandamano ya kupinga kuungwa mkono Israel yameongezeka barani Ulaya?
Sep 15, 2025 11:00Maelfu ya watu wamemiminika barabarani mjini Berlin kupinga sera za Ujerumani katika eneo la Asia Magharibi hususan za kuunga mkono jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Rais wa zamani wa Ireland: Nikiwa raia wa Ulaya 'naona aibu' kwa namna EU inavyoamiliana na Israel
Sep 14, 2025 11:02Rais wa zamani wa Ireland Mary Robinson amesema, "anaona aibu" kwa mjibizo ambao Umoja wa Ulaya (EU) umeonyesha kwa vita vinavyoendelezwa na Israel huko Ghaza, na akaukosoa umoja huo kwa kushindwa kusimamisha makubaliano yake ya kibiashara na utawala huo wa kizayuni licha ya wito uliotolewa wa kuutaka ufanye hivyo.
-
Bunge la Ulaya lataka kutambuliwa rasmi Palestina Huru
Sep 12, 2025 06:37Bunge la Ulaya limepasisha azimio likielezea wasiwasi wake kuhusu hali mbaya ya Ukanda wa Gaza, na kuzitaka nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya kuliweka suala la kutambuliwa taifa huru la Palestina kwenye ajenda.
-
Iran yapongeza mazungumzo 'yenye tija' ya Araghchi na Kallas, yaihimiza EU iachane na mtazamo wa makabiliano
Sep 09, 2025 11:06Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema, mkutano wa Waziri wa Mambo ya Nje Abbas Araghchi na Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas ulikuwa wenye tija, na kubainisha kuwa hoja na rai mbalimbali ziliwasilishwa katika mazungumzo yao.
-
"Vikwazo vya Marekani, Ulaya vimeua watu milioni 38 tangu 1970"
Sep 04, 2025 07:42Tahariri iliyoandikwa na tovuti ya habari ya kanali ya televisheni ya al-Jazeera ya Qatar imekosoa muenendo wa nchi za Magharibi kutumia vikwazo kuziadhabu nchi zinazozitazama kama maadui; ikieleza kuwa, vikwazo vya Marekani na Umoja wa Ulaya vimeua watu zaidi ya milioni 38 kote duniani tangu 1970.