Pars Today
Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ametahadharisha kuwa umoja huo unakabiliwa na chuki zinazoongezeka katika Ulimwengu wa Kiislamu na nje yake kutokana na shutuma za kuegemea upande wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kuwa na misimamo ya undumilakuwili kuhusiana na Vita vya Gaza.
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema kuwa, matamshi ya mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya dhidi ya makundi ya muqawama ni kupindua uhakika wa mambo na ni kujaribu kufunika jinai za utawala wa Kizayuni.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya zimepoteza takriban dola trilioni 1.5 kutokana na vikwazo vya Wamagharibi dhidi ya Moscow.
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni kwenye maeneo ya makazi ya watu, vituo vya matibabu na skuli za Ghaza yanakanyaga sheria za kimataifa na utu na ubinadamu.
Baada ya kuanza oparesheni kwa jina la "Kimbunga cha Al Aqsa" iliyotekelezwa na Hamas na makundi mengine ya mapambano ya Palestina; serikali na vyombo vya habari vya Magharibi kwa upande mmoja vimeanzisha propaganda kubwa ili kuzuia kuakisiwa habari na matukio yanayojiri huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu huku vikichapisha na kutoa habari za uwongo ili kuonyesha taswira isiyo ya kibinadamu kuhusu wanamapambano wa Palestina.
Umoja wa Ulaya umesema kuwa utawala wa Israel umekiuka sheria za kimataifa kwa kuuweka Ukanda wa Gaza chini ya mzingiro.
Hitilafu kuhusu kadhia ya wahamiaji miongoni mwa nchi za Umoja wa Ulaya zingali zinaendelea licha ya makubaliano ya hivi karibuni kuhusu suala hilo.
Rais Kais Saied wa Tunisia amekataa kupokea msaada wa kifedha wa Umoja wa Ulaya (EU) uliokusudia kupiga jeki bajeti ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika, sanjari na kuisaidia kukabiliana na mgogoro wa wakimbizi.
Josep Borrell Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ametahadharisha kuwa umoja huo unakabiliwa na mgawanyiko mkubwa kuhusu sera za uhamiaji na kwamba suala hilo linaweza kuufanya Umoja wa Ulaya uvunjike.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo kwa hatua ya kujikariri ya Umoja wa Ulaya na Uingereza ya kuendelea kulisakama taifa hili kwa vikwazo.