Mar 28, 2023 07:25
Jopo la uchunguzi la Umoja wa Mataifa limesema kwamba, kuna ushahidi unaoonyesha kuwa jinai dhidi ya binadamu zimefanywa dhidi wa wananchi wa Libya na wahajiri waliokwama katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika, wakiwemo wanawake wanaolazimishwa kuingia kwenye utumwa wa kingono.