-
Rouhani: Mazungumzo ya Astana na Sochi yameleta matumaini ya usalama na uthabiti wa Syria
Feb 20, 2018 00:35Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ushirikiano na mazungumzo ya pande tatu ya Iran, Russia na Uturuki kuhusiana na masuala ya Mashariki ya Kati, hususan vita dhidi ya ugaidi na kupatiwa ufumbuzi mgogoro wa Syria yamekuwa na taathira chanya na amesisitiza juu ya kuendelezwa juhudi na ushirikiano huo ili kufikiwa malengo kusudiwa.
-
Jeshi la Uturuki lashambulia kwa makombora maeneo ya makazi ya raia mjini Afrin, Syria
Feb 14, 2018 13:05Katika kuendelea na operesheni za kijeshi za Uturuki kaskazini mwa Syria, jeshi la nchi hiyo limeshambulia kwa makombora maeneo ya makazi ndani ya mji wa Afrin.
-
Mvutano katika uhusiano wa Misri na Uturuki
Feb 07, 2018 11:19Uhusiano wa Misri na Uturuki umeharibika kuhusiana na suala la uchoraji mipaka katika Bahari ya Mediterania.
-
Qassemi: Iran haitakubali sharti lolote lile kuhusiana na safari ya Rais wa Ufaransa mjini Tehran
Feb 05, 2018 13:01Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran haitakubali sharti lolote lile kwa ajili ya safari ijayo ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa hapa nchini.
-
Wapinzani Uturuki: Siasa za ndani na nje za serikali ya Erdoğan zimefeli sana
Jan 31, 2018 11:52Naibu Mkuu wa Chama cha Upinzani cha Saadet nchini Uturuki amesema kuwa, siasa za kigeni na ndani za serikali ya Rais Recep Tayyip Erdoğan zimefeli kwa kiasi kikubwa.
-
Boroujerdi: Marekani inaendelea kuwaunga mkono magaidi Syria
Jan 28, 2018 11:41Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa ya Siasa za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, vitendo vya Marekani zinaonesha kuwa Washington ingali inaunga mkono ugaidi na vitendo vya kuvuruga amani na utulivu pamoja na kutaka kuzigawa vipande vipande nchi za eneo hili ikiwemo Syria.
-
Ndege ya kivita ya Uturuki yatunguliwa Afrin, Wakurdi wakaribisha kurudi jeshi la Syria
Jan 25, 2018 10:34Mmoja wa makamanda wa ngazi ya juu wa kundi la wapiganaji wa Kikurdi katika eneo la Afrin, Syria amekaribisha kuingia jeshi la nchi hiyo katika eneo hilo na kusisitiza kuwa, serikali ya Damascus imefikia makubaliano kadhaa na viongozi wa kundi hilo.
-
Libya yaituhumu Uturuki kuhusika na miripuko ya mabomu iliyotokea Benghazi
Jan 25, 2018 00:19Msemaji wa jeshi la taifa la Libya ameituhumu Uturuki kuwa imehusika na miripuko ya mabomu iliyotokea mjini Benghazi mashariki mwa Libya.
-
Polisi ya Uturuki yawatawanya waandamanaji wanaopinga uvamizi wa nchi hiyo huko Syria
Jan 22, 2018 04:14Polisi ya Uturuki imetumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliomiminika barabarani kupinga uvamizi wa jeshi la nchi hiyo katika mji wa Afrin, kaskazini mwa Syria.
-
Rais Assad aishukuru Iran kwa msaada wake kwa Syria
Jan 21, 2018 23:33Rais wa Syria ameishukuru Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa uungaji mkono wake kwa taifa la Syria na kusema: "Istikama ya wanajeshi Wairani na waitifaki wao katika medani ya vita ni jambo ambalo limetoa mchango mkubwa katika ushindi wa jeshi na taifa la Syria."