May 24, 2020 08:55
Katika hali ambayo ikulu ya Marekani ya White House inatekeleza vikwazo vikali zaidi vilivyo kinyume na ubinaadamu dhidi ya raia na serikali ya Venezuela kwa lengo la kuiondoa madarakani serikali halali ya Rais Nicolás Maduro, kuongezeka ushirikiano wa kibiashara kati ya Tehran na Caracas na kutumwa meli za mafuta zilizosheheni nishati hiyo muhimu huko Venezuela, kumewaongezea hasira viongozi wa Marekani.