-
WHO: Ukatili dhidi ya wanawake ungali ni janga kubwa la haki za binadamu
Nov 20, 2025 06:08Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO) pamoja na wadau wa Umoja wa Mataifa wametoa ripoti muhimu inayoonyesha kuwa ukatili dhidi ya wanawake ungali ni janga kubwa la haki za binadamu, kwa sababu takwimu za zaidi ya miaka 20 zinaonesha kutokuwepo kwa hatua kubwa zilizopigwa katika kupunguza ukatili huo.
-
UN: Raia 114 wameuawa Lebanon katika ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa na Israel
Nov 14, 2025 02:37Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema ukiukaji wa usitishaji vita uliofanywa Israel uliotokana na makubaliano yaliyofikiwa kati ya utawala huo wa kizayuni na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon ya Hizbullah mnamo Novemba 2024 umesababisha vifo vya raia 114 wa nchi hiyo.
-
Umoja wa Mataifa watahadharisha kuhusu hatari ya njaa katika nchi 16
Nov 14, 2025 02:25Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na Mpango wa Chakula Duniani (WFP) zimeonya kuhusu mgogoro mkubwa wa ukosefu wa usalama wa chakula unaozidi kuwa mbaya katika nchi 16, na kuweka hatarini maisha ya mamilioni ya watu, hasa katika maeneo yenye migogoro na majanga ya hali ya hewa.
-
UN: Mashambulizi ya walowezi wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukingo wa Magharibi yamefikia kiwango cha juu zaidi
Nov 08, 2025 07:57Umoja wa Mataifa umetangaza kwamba walowezi wa Israel wamefanya mashambulizi yasiyopungua 264 dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu mwezi uliopita wa Oktoba, ikiwa ni idadi kubwa zaidi ya kila mwezi tangu maafisa wa Umoja wa Mataifa walipoanza kufuatilia mashambulizi kama hayo mwaka 2006.
-
UN: Israel imekataa maombi zaidi ya 100 ya kuingiza misaada Ghaza tangu vita viliposimamishwa
Nov 07, 2025 10:17Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, tangu yalipoanza kutekelezwa makubaliano ya kusitisha vita tarehe 10 Oktoba, utawala wa kizayuni wa Israel umekataa maombi 107 ya kuingizwa vifaa vya misaada katika Ukanda wa Ghaza, na hivyo kuzuia vifaa muhimu vya kibinadamu kuwafikia Wapalestina wa eneo hilo wanaoishi katika mazingira magumu na ya mateso.
-
UNSC yapitisha azimio la US la kuunga mkono mpango wa Morocco kuhusu Sahara Magharibi
Nov 02, 2025 06:23Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepiga kura ya kurefusha kwa mwaka mmoja muda wa kazi za ujumbe wake ulioko Sahara Magharibi (MINURSO), sambamba na kuidhinisha rasmi mpango wa serikali ya Morocco wa kutoa mamlaka ya ndani kwa eneo hilo kama msingi pekee wa kutatua mgogoro huo wa miongo kadhaa, hatua ambayo imesababisha mpasuko mkubwa katika jamii ya kimataifa.
-
Araghchi na Guterres wajadili migogoro ya Gaza, Yemen
Oct 21, 2025 11:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres wamefanya mazungumzo ya simu na kuzungumzia matukio ya kikanda ikiwemo hali ya Gaza na Yemen.
-
UN: Makubaliano ya amani ya Kongo na Rwanda 'hayaheshimiwi'
Oct 14, 2025 12:47Umoja wa Mataifa umesema kuwa makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rwanda "hayaheshimiwi."
-
Umoja wa Mataifa wakaribisha taarifa ya Hamas kuhusu usitishaji vita Gaza
Oct 04, 2025 07:31Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekaribisha kwa mikono miwili taarifa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas inayoonyesha utayarifu wake wa kuwaachilia mateka na kukubali kwa masharti mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump wa kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Je, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limenasa katika mtego wa kura ya turufu?
Oct 01, 2025 02:32Haki ya kura ya turufu ni mojawapo ya masuala yenye utata kuhusu mamlaka ya wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.