Mar 20, 2024 11:32
Utumikishaji binadamu kwenye sekta ya uchumi binafsi ikiwemo biashara ya ngono, viwandani na kwenye mashamba huingiza dola bilioni 236 za faida isiyo halali kila mwaka. Hayo yameelezwa katika ripoti mpya na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi Duniani, ILO.