-
Pande hasimu Sudan zatakiwa kulinda usalama wa raia
Apr 11, 2025 07:26Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) imezitaka pande hasimu nchini Sudan kulinda usalama wa raia na kurahisisha kufikiwa na misaada ya kibinadamu maeneo ya mapigano ili kuepusha majanga zaidi ya kibinadamu nchini humo.
-
Serikali ya Sudan yakanusha madai ya kutuma mjumbe huko Israel
Apr 11, 2025 04:12Serikali ya Sudan imekanusha kwamba imetuma mjumbe Israel, kufuatia ripoti kwamba mkuu wa Baraza la Mpito la Utawala wa Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, alimtuma mjumbe kukutana na maafisa wa serikali ya Tel Aviv.
-
Ennahda ya Tunisia yataka kuachiliwa wafungwa wa kisiasa walio kwenye mgomo wa kula
Apr 11, 2025 04:10Harakati ya upinzani nchini Tunisia ya Ennahda imetoa wito kwa serikali ya nchi hiyo kuwaachilia huru wafungwa wa kisiasa wanaogoma kula.
-
Reuters: Wawawakilishi wa serikali ya Kongo DR na waasi wa M23 wawasili Doha kwa mazungumzo
Apr 10, 2025 23:26Shirika la habari la Reuters limeripoti kuwa maafisa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wawakilishi wa harakati ya waasi ya M23 wamewasili Doha kwa mazungumzo yenye lengo la kufikia makubaliano ya kusitisha vita na kumaliza mapigano ya miezi kadhaa mashariki kwa Kongo DR.
-
Sudan yaiambia ICJ kuwa UAE inachochea mauaji ya halaiki Darfur
Apr 10, 2025 22:36Sudan iliiambia Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) jana Alhamisi kwamba, Umoja wa Falme za Kiarabu umekiuka Mkataba wa Mauaji ya Kimbari kwa kuunga mkono vikosi vya wanamgambo huko Darfur, na kuwataka majaji wa mahakama hiyo kutoa amri ya dharura ya kuzuia mauaji ya kimbari katika eneo hilo.
-
Ethiopia yataka Italia irejeshe mali ilizopora za Shujaa wa Vita Ras Desta Damtew
Apr 10, 2025 04:14Serikali ya Ethiopia imezindua kampeni maalum ya kurejesha mali za kihistoria na kiutamaduni zilizoporwa na utawala wa kikoloni wa Italia, mali ambazo zilikuwa zikimilikiwa na shujaa wa vita wa taifa hilo, Ras Desta Damtew.
-
Machar apokonywa uongozi wa upinzani Sudan Kusini akiwa kizuizini
Apr 10, 2025 04:14Chama kikuu cha upinzani nchini Sudan Kusini, Sudan People’s Liberation Movement-in-Opposition (SPLM-IO), siku ya Jumatano kilimteua mwenyekiti wa mpito huku Makamu wa Kwanza wa Rais wa chama hicho, Riek Machar, akiendelea kuzuiliwa nyumbani.
-
Afrika yashuhudia kupungua vifo vya akina mama na watoto wachanga
Apr 09, 2025 23:25Viwango vya vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga barani Afrika vimepungua tangu mwaka 2000, Shirika la Afya Duniani (WHO) limebaini katika ripoti mpya.
-
Kadhaa wauawa katika shambulizi la kigaidi kaskazini mwa Msumbiji
Apr 09, 2025 23:24Watu wasiopungua watano wameuawa huku wengine kadhaa wakijeruhiwa vibaya katika shambulio la kigaidi katika jimbo la Cabo Delgado, kaskazini mwa Msumbiji.
-
Wanahabari Nigeria wataka Israel iwekewe vikwazo vya mafuta, gesi
Apr 09, 2025 23:23Mwenyekiti wa Muungano wa Waandishi wa Habari wa Nigeria (NUJ), Ibrahim Muhammad, ametoa wito kwa nchi za Kiislamu kuungana na kutumia nguvu zao za kiuchumi, hususan mafuta na gesi, kama nyenzo ya kukomesha mauaji ya kimbari ya Israel na Marekani huko Palestina na kwingineko.