-
Equatorial Guinea yaishtaki Ufaransa kwa mahakama ya UN kwa uporaji
Jul 05, 2025 11:53Equatorial Guinea imewasilisha kesi dhidi ya Ufaransa katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki ikitaka kusitishwa uuzaji wa jumba la kifahari mjini Paris, ambalo nchi hiyo ya Afrika Magharibi inataka kulitwaa tena, mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ilisema hayo jana Ijumaa.
-
Rais wa Rwanda asema hana uhakika wa kufanikiwa makubaliano ya amani ya DRC
Jul 05, 2025 03:49Rais Paul Kagame wa Rwanda amekaribisha kwa tahadhari makubaliano ya amani yaliyofikiwa kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC na kundi la waasi la M23 kwa upatanishi wa Marekani akisema, kufanikiwa kwa mapatano hayo kunategemea nia njema itakayoonyeshwa na pande husika.
-
Rais Ruto akiri kujenga kanisa ndani ya Ikulu ya Rais, asema: Sitaomba msamaha
Jul 04, 2025 11:53Rais William Ruto wa Kenya amekiri kuwa anajenga Kanisa katika Ikulu ya Rais akidai kuwa anatumia pesa zake kujenga kanisa hilo.
-
Rais wa Afrika Kusini: Mazungumzo ya kitaifa yataendelea bila mshirika wa muungano
Jul 04, 2025 11:49Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amesema kuwa mazungumzo ya kitaifa yenye lengo la kuimarisha umoja na kuiunganisha nchi baada ya uchaguzi wa mwaka jana yataendelea bila mshirika mkuu katika serikali ya mseto ya nchi hiyo.
-
Waasi wa M23: Tuko tayari kushiriki mazungumzo ya amani ya Doha
Jul 04, 2025 03:42Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na waasi wa M23 wamesema kwamba watatuma wajumbe nchini Qatar kwa mazungumzo ya amani, huku Washington ikishinikiza kukomeshwa kwa mapigano ambayo yanaweza kusaidia kufungua mabilioni ya uwekezaji katika madini.
-
Madaktari Wasio na Mipaka waonya kuhusu uhalifu dhidi ya raia al-Fasher Sudan
Jul 04, 2025 03:31Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) lina wasiwasi kuhusu uwezekano wa kutokea mashambulizi makubwa katika mji wa al-Fasher na umwagaji damu unaoweza kusababisha, huku mamia kwa maelfu ya raia wakiwa wamekwama katika mji huo.
-
Serikali ya Tanzania yakanusha madai ya kupanga kumpa sumu Tundu Lissu
Jul 04, 2025 00:15Serikali ya Tanzania imekanusha vikali tuhuma zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii na kudai kuwa zinaihusisha yenyewe na kiongozi wa upinzani, Tundu Antipas Lissu, katika mpango wa kumuwekea sumu mshtakiwa huyo.
-
Abiy Ahmed atangaza kukamilika Bwawa la Renaissance, azialika Misri na Sudan katika sherehe za ufunguzi
Jul 03, 2025 23:41Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed, ametangaza "kukamilika kazi" katika mradi wa Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD) kwenye Mto Nile, akisema litazinduliwa mwezi Septemba. Vilevile ametoa wito kwa Misri, Sudan, na watu wa Bonde la Mto Nile kuungana katika kusherehekea "hatua hiyo ya kihistoria."
-
Chama cha siasa cha '47 Voices of Kenya Congress', chaingia rasmi kwenye uwanja wa siasa
Jul 03, 2025 08:34Chama kipya cha kisiasa kinachoongozwa na vijana kilichopewa jina ‘47 Voices of Kenya Congress', kimeingia rasmi kwenye uwanja wa siasa nchini humo. Hali hiyo inapelekea kuujitokeza sura mpya katika siasa za vijana wa Kenya maarufu kama Gen Z.
-
Jeshi la Mali: Zaidi ya magaidi 80 wauawa katika mashambulizi yaliyoratibiwa nchini humo
Jul 03, 2025 00:30Magaidi zaidi ya 80 wameuawa katika mashambulizi yaliyolenga maeneo kadhaa ya katikati na magharibi mwa Mali.