-
Serikali ya Somalia yathibitisha kuuawa kwa magaidi wa Al-Shabab katika shambulio la gereza jijini Mogadishu
Oct 05, 2025 07:10Serikali ya Somalia imethibitisha kuwa wapiganaji saba wa kundi la kigaidi la Al-Shabab wanaofungamana na kundi la kigaidi la al-Qaeda wameuawa baada ya makabiliano ya saa kadhaa kufuatia shambulio kubwa dhidi ya gereza la Godka Jilow mjini Mogadishu, tukio ambalo ni miongoni mwa mashambulizi makubwa zaidi katika mji mkuu kwa miezi ya hivi karibuni.
-
Waandamanaji nchini Morocco: Tunahitaji zaidi hospitali kuliko viwanja vya soka
Oct 05, 2025 04:07Makabiliano makali yanaripotiwa kutokea baina ya waandamanaji na vyombo vya usalama nchini Morocco.
-
Wanamgambo washambulia gereza katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu
Oct 05, 2025 04:06Sauti za milipuko na risasi zilisikika pakubwa jana huko Mogadishu mji mkuu wa Somalia baada ya wanamgambo kushambulia gereza karibu na ikulu ya rais.
-
Madagascar: Rais Rajoelina alaani jaribio la mapinduzi dhidi ya serikali yake
Oct 04, 2025 22:57Rais Andry Rajoelina wa Madagascar ambaye serikali yake inakabiliwa na mashinikizo makuubwa ya maandamano amelaani kile alichokiita jaribio la mapinduzi dhidi ya serikali yake.
-
Waandamanaji wa Afrika Kusini wataka Israel iwaachilie wanaharakati wa msafara wa Gaza
Oct 04, 2025 07:45Waandamanaji waliokusanyika nje ya ubalozi wa utawala wa Israel nchini Afrika Kusini siku ya Ijumaa wametoa wito wa kuachiliwa kwa wanaharakati raia wa Afrika Kusini na wengine wote waliotekwa nyara na majeshi ya Israel wakiwa katika msafara wa meli unaojulikana kama Sumud uliokuwa ukielekea Gaza kupelekea misaada ya kibinadamu.
-
Misri yaituhumu Ethiopia kwa usimamizi mbovu wa Bwawa la GERD ambao umesabisha mafuruko
Oct 04, 2025 07:40Serikali ya Misri imeituhumu Ethiopia kuwa imefanya 'uzembe na haina uwajibikaji” katika usimamizi wa mafuriko ya Mto Nile kupitia uendeshaji wa upande mmoja wa bwawa lake kubwa, ikisema hatua hizo zimeongeza mafuriko nchini Sudan na kutishia moja kwa moja ardhi na maisha ya Wamisri, huku mgogoro wa muda mrefu kuhusu bwawa hilo linalojulikana kama Grand Ethiopian Renaissance Dam (GERD) ukishaidi.
-
WFP yaonya kuhusu hali ya janga nchini Somalia huku ufadhili ukizidi kupungua
Oct 04, 2025 07:34Mamilioni ya watu nchini Somalia wanakabiliwa na njaa inayozidi kuwa mbaya, kufuatia kupunguzwa kwa misaada ya wafadhili, hali inayoliweka shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) katika upungufu mkubwa wa ufadhili.
-
Jeshi la Sudan: Mamluki wa Kiukraine wanaounga mkono waasi wa RSF wauawa vitani
Oct 04, 2025 07:21Jeshi la Sudan limetangaza kuuawa kwa idadi kubwa ya wapiganaji wa kigeni, wakiwemo mamluki wa Kiukraine, waliokuwa wakiunga mkono kikosi cha waasi cha Rapid Support Forces (RSF) katika vita vya muda mrefu vya ndani nchini humo.
-
Wanigeria waandamana kulaani shambulio la Israel dhidi ya msafara wa Sumud
Oct 04, 2025 02:34Waislamu kote nchini Nigeria waliingia barabarani baada ya Swala ya Ijumaa hapo jana kulaani shambulio la Israel dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumud, wenye makumi ya meli zinazoelekea katika Ukanda wa Gaza.
-
Mafuriko yaua 19 Sudan Kusini, malaki waachwa bila makazi
Oct 04, 2025 02:26Mafuriko makubwa yaliyosababishwa na mvua kubwa nchini Sudan Kusini yamesababisha vifo vya watu 19 na kuathiri wengine karibu 640,000 katika kaunti 26 katika majimbo sita ya nchi hiyo, hayo yamesemwa na Umoja wa Mataifa.