-
Iran yalaani shambulizi la waasi dhidi ya Msikiti nchini Sudan
Sep 22, 2025 04:08Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali shambulizi la droni lililotokea hivi karibuni katika msikiti wa Al-Fashir, Sudan, ambalo limesababisha vifo na majeruhi kwa makumi ya waumini wa Kiislamu wasio na hatia.
-
Jeshi la Somalia laua magaidi wanne wa al-Shabaab
Sep 22, 2025 03:49Jeshi la taifa la Somalia, kwa kushirikiana na washirika wa kimataifa, limeendesha operesheni iliyopangwa kwa umakini na kuwaua angalau wapiganaji wanne wa kundi la kigaidi la al-Shabaab, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani vilivyoripoti Jumapili.
-
Takriban magaidi 34 wauawa katika operesheni za kijeshi za Niger
Sep 21, 2025 23:13Jeshi la Niger limetangaza kuwa, Vikosi vya Ulinzi na Usalama vya nchi hiyo vimeangamiza magaidi wasiopungua 34 wakati wa operesheni mbili zilizofanywa wiki iliyopita katika mikoa ya magharibi ya Dosso na Tillabery ya nchi hiyo.
-
Majaliwa: Rais Samia anatambua mchango wa madhehebu ya dini katika kuendeleza maarifa
Sep 21, 2025 03:21Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua kwa dhati mchango wa madhehebu ya dini likiwemo Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) na wadau wote wa elimu katika kuimarisha maadili, kuendeleza maarifa na kuleta mshikamano wa kitaifa kupitia elimu.
-
Polisi Malawi yawatia mbaroni maafisa wa uchaguzi kwa madai ya udukuzi wa data
Sep 21, 2025 03:20Polisi nchini Malawi imewatia mbaroni maafisa wanane wa uchaguzi wanaotuhumiwa kujaribu kudukua matokeo ya uchaguzi wakati zoezi la kuhesabu kura likiendelea kufuatia ucaguzi mkuu wa Jumanne iliyopita nchini humo.
-
Sudan yawashutumu RSF kufanya mauaji ya umati Msikitini huko El Fasher
Sep 20, 2025 23:34Serikali ya Sudan imewashutumu wapiganaji wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) kuwa wameshambulia kwa makusudi Msikiti mmoja huko El Fasher, makao makuu ya jimbo la Darfur Kaskazini na kuua zaidi ya Waislamu 70 wakati wa Sala ya Alfajiri.
-
Ongezeko la ghasia mashariki mwa DRC laongeza mahitaji ya vifaa vya dharura
Sep 20, 2025 23:04Ghasia na machafuko yanaendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, suala ambalo limezidisha maafa na matatizo kwa raia wa kawaida hasa wanawake na watoto wadogo.
-
Polisi Afrika Kusini yahimiza kupambana vilivyo na magenge ya Cape Magharibi
Sep 20, 2025 23:03Kaimu Waziri wa Polisi wa Afrika Kusini, Firoz Cachalia ametoa mwito kwa wananchi kulisaidia kikamilifu jeshi hilo katika kuweka ulinzi mkali wa kipolisi na uwekezaji wa kijamii ili kuzuia kuongezeka ghasia za magenge ya wahalifu kwenye Jimbo la Cape Magharibi.
-
Waasi washambulia mji wa mpakani wa Nigeria, wanajeshi watimua mbio na kuingia Cameroon
Sep 20, 2025 08:02Waasi wameshambulia mji mmoja wa mpakani katika jimbo la Borno, kaskazini mwa Nigeria na kuchukua silaha katika kambi ya kijeshi katika eneo hilo huku wanajeshi wakikimbilia usalama wao katika nchi jirani. Hayo yamesemwa na wakazi na maafisa wa usalama katika eneo la tukio. Tukio hilo limeripotiwa katika mji wa Banki, katika wilaya ya Bama.
-
Mzozo wa kidiplomasia waendelea kutokota baina ya Mali na Ufaransa
Sep 20, 2025 04:22Ufaransa imeamuru wanadiplomasia wawili wa Mali kuondoka nchini humo, kufuatia kukamatwa kwa mwanadiplomasia wake nchini Mali mwezi Agosti.