-
UN: Zaidi ya watu 110 wafariki au kupotea katika ajali za wakimbizi pwani ya Libya
Sep 20, 2025 04:16Ajali mbili za baharini karibu na pwani ya Libya zimeacha zaidi ya wakimbizi 110 wa Kisudan wakiwa wamefariki au hawajulikani walipo, kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa.
-
Watu 8 wauawa katika mapigano baina ya wafuasi wa kundi la Wazalendo mashariki mwa DRC
Sep 20, 2025 04:12Makundi mawili ya wanamgambo wa Wazalendo, yanayoongozwa na majenerali wanaojiita Malaika na Nyakiliba, yamekuwa yakipambana tangu Septemba 17 katika eneo la Mwenga, mkoani Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wakiwania udhibiti wa mji wa kimkakati.
-
Algeria: Kuna hatari UNSC likashindwa kwa mara ya tatu kuzuia mauaji ya kimbari kufuatia kura ya veto ya US
Sep 19, 2025 23:09Algeria imelitahadharisha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba linakabiliwa na hatari ya kukariri kushindwa kwake mtawalia katika miaka ya nyuma kuzuia mauaji ya kimbari baada ya Marekani kwa mara ya sita kutumia kura yake ya veto kupinga azimio lililoungwa mkono na nchi 14 wanachama kati ya nchi 15 wa UNSC.
-
Taasisi ya misaada Sudan: Shambulio la RSF limeua watu 75 Darfur
Sep 19, 2025 23:07Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF vimewaua watu 75 katika shambulio la ndege zisizo na rubani lililolenga msikiti mmoja katika kambi ya watu waliolazimika kuyahama makazi yao kwenye jimbo la Darfur nchini Sudan. Hayo yameelezwa na taasisi ya utoaji misaada inayoendesha eneo hilo inayojulikana kama Chumba cha Mjibizo wa Dharura (Emergency Response Room).
-
Gbagbo aapa kutomuunga mkono mgombea yeyote katika kinyang'anyiro cha urais wa Ivory Coast
Sep 19, 2025 23:06Laurent Gbagbo Rais wa zamani wa Ivory Coast amesema hatomuunga mkono mgombea yeyote katika uchaguzi ujao wa rais.
-
Kuanzia kupambana na ubaguzi wa rangi hadi kushirikiana na wavamizi; Nigeria inaelekea wapi?
Sep 19, 2025 11:37Nigeria imesimama na mataifa yanayodhulumiwa katika miongo kadhaa iliyopita, hasa katika mapambano dhidi ya utawala wa kibaguzi nchini Afrika Kusini, na imetetea misingi ya haki na kupinga ukoloni.
-
Kampeni za Kura ya Maoni ya Katiba nchini Guinea Conakry zakamilika bila ya kuwepo upinzani
Sep 19, 2025 07:34Mji mkuu wa Guinea, ulikuwa na shughuli nyingi jana Alkhamisi, ambayo ilikuwa siku ya kufunga kampeni kabla ya kufanyika kura ya maoni ambayo itaweza kumruhusu kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi yaliyofanyika nchini humo miaka mitatu iliyopita kuwania urais.
-
Uchaguzi Malawi: Wagombea wawili wakuu wa urais kila mmoja ajitangazia ushindi
Sep 19, 2025 03:25Vyama vya wagombea wawili wakuu katika uchaguzi wa rais nchini Malawi vimejitangazia ushindi na kuzua wasiwasi wa kuibuuka mzozo.
-
WHO: Zaidi ya watu 30 wamekufa kwa Ebola Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
Sep 19, 2025 03:24Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, maambukizi 48 ya ugonjwa wa Ebola yamethibitishwa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na watu 31 wamefariki dunia.
-
Riek Machar aiweka njia panda Sudan Kusini
Sep 19, 2025 03:23Upinzani nchini Sudan Kusini umetoa wito wa "mabadiliko ya utawala" dhidi ya serikali ya Rais Salva Kiir baada ya miezi kadhaa ya kuvunjika kwa makubaliano ya kugawana madaraka mwaka 2018 na Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar.