-
Baqaei: Marekani na Magharibi zimehusika katika mauaji ya Israel ya waandishi wa habari huko Gaza
May 04, 2025 04:17Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amesema kuwa, mwenendo wa utawala wa Israel wa kuwalenga waandishi wa habari wa Kipalestina umewezeshwa na msaada usiosita wa waungaji mkono wake wa Magharibi, hususan Marekani.
-
Baqaei: Mashambulizi ya Israel dhidi ya "Meli ya Dhamiri " ni kitendo cha kigaidi dhidi ya usalama wa baharini
May 03, 2025 23:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, shambulio la ndege zisizo na rubani za utawala wa Israel dhidi ya meli iliyokuwa imebeba misaada ya kibinadamu kwa ajili ya watu wa Gaza ni jinai ya wazi dhidi ya watu wa Palestina na ni kitendo cha kigaidi dhidi ya usalama wa baharini.
-
Araghchi: Mienendo inayokinzana ya Marekani inazidisha kutoaminiwa diplomasia
May 03, 2025 08:24Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mienendo inayokinzana ya Marekani ndio sababu ya kuongezeka kutoaminiana katika uga wa diplomasia.
-
Sisitizo la Iran la kufikiwa makubaliano ya nyuklia ya haki na yenye uwiano
May 03, 2025 07:29Kufuatia kuakhirishwa duru ya nne ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani, Sayyid Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa, Tehran imeazimia kufikia makubaliano ya haki na yenye mlingano kuliko wakati mwingine wowote.
-
Araghchi asisitiza: Iran ina haki ya kumiliki mzunguko kamili wa fueli ya nyuklia
May 03, 2025 03:27Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema, kurudia kila mara kauli za uwongo hakubadilishi ukweli wa kimsingi na akaeleza bayana kwamba, Iran, ikiwa ni miongoni mwa nchi zilizotia saini mkataba wa NPT, ina haki ya kumiliki mzunguko kamili wa fueli ya nyuklia.
-
Iran yalaani jinai za kivita za Marekani nchini Yemen
May 02, 2025 23:13Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amelaani vikali wimbi la mashambulizi ya jeshi la Marekani katika muda wa saa 24 zilizopita katika maeneo mbalimbali ya majimbo ya Sana'a, Saada, na Al-Jawf nchini Yemen, yakilenga miundombinu na maeneo ya makazi ya Yemen.
-
Seddiqi: Teknolojia ya nyuklia ni mtaji wa taifa/kuna udharura wa kuwaheshimu walimu na wafanyakazi
May 02, 2025 07:44Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo ya hapa mjini Tehran ameashria mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja ya nyuklia kati ya Iran na Marekani yaliyoanza wiki kadhaa zilizopita na kusema: Timu ya mazungumzo ya Iran ina uzoefu mkubwa; na katika mazungumzo hayo inatetea kwa nguvu na irada kamili haki ya Iran ya kumiliki teknolojia ya amani ya nyuklia ambayo ni mtaji wa taifa.
-
Araghchi: Iran imeazimia kikweli kufikia makubaliano yenye uwiano
May 02, 2025 07:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi amesema kuwa Iran hivi sasa imeazimia kikwelikweli kufikia makubaliano ya haki na yenye uwiano kuliko wakati mwingine wowote.
-
Mkuu wa Kamati ya Bunge ya Usalama wa Taifa Iran ajibu vitisho vya Waziri wa Ulinzi wa Marekani
May 02, 2025 04:09Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu amejibu vitisho vya Waziri wa Ulinzi wa Marekani akisema kuwa, Wamarekani wenyewe ndio watakaolipa gharama ya mienendo yao inayokinzana.
-
Baqaei atangaza mabadiliko katika ratiba ya mazungumzo ya Iran na Marekani
May 02, 2025 03:54Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza kubadilishwa tarehe ya duru ijayo ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja ya Iran na Marekani ambayo yalipangwa kufanyika Jumamosi ya tarehe 4 Mei huko Roma, mji mkuu wa Italia.