-
Trump azitaka kampuni za US zitengeneze droni kama za Iran
May 16, 2025 03:31Rais wa Marekani, Donald Trump amesema ameziomba kampuni za Marekani kutengeneza ndege zisizo na rubani zinazofanana na droni za Iran, ambazo si ghali sana bali zina kasi ya juu na hatari.
-
Spika Qalibaf: Iran, Algeria zinahitaji kufanya kazi kusaidia usambazaji wa misaada Gaza
May 15, 2025 08:31Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf amesema Iran na Algeria zinahitaji kufanya kazi ili kusaidia juhudi za kufikisha misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza uliokumbwa na vita.
-
Iran yahimiza kukomeshwa ghasia katika mji mkuu wa Libya, Tripoli
May 15, 2025 08:14Iran imeelezea wasiwasi wake kuhusu mapigano makali yanayoendelea kati ya makundi yenye silaha katika mji mkuu wa Libya Tripoli, ikitaka kusitishwa mara moja ghasia na umwagaji damu.
-
Umuhimu wa kufanyika Kongamano la 31 la Nyuklia la Iran
May 15, 2025 04:32Kongamano la 31 la Nyuklia la Iran linafanyika katika mji mtakatifu wa Mashhad, na kuhudhuriwa na wasomi wa kisayansi, sekta binafsi na wasomi vijana wa Iran.
-
Pezeshkian amjibu Trump: Inaonekana huwajui kabisa Wairani
May 15, 2025 04:09Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amejibu kauli za Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Iran na kusema kuwa, inaonekiana kiongozi huyo wa Marekani hawafahamu wananchi wa Iran.
-
Spika Qalibaf: Maendeleo ya ulimwengu wa Kiislamu yanategemea ushirikiano wa Iran na Saudi Arabia
May 15, 2025 04:08Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya ulazima wa kuwepo umoja baina ya nchi za Kiislamu na kubainisha kwamba, Iran na Saudi Arabia zinapaswa kutumia fursa iliyojitokeza kuendeleza uhusiano wao sambamba na maendeleo ya Ulimwengu wa Kiislamu.
-
Kiongozi Muadhamu: Iran ina wajibu wa kusimama dhidi ya tawala kandamizi
May 15, 2025 01:10Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema lazima Iran isimame dhidi ya tawala zinazoua watoto pamoja na wale wanaowaunga mkono na kusitisha ukandamizaji, na itaendelea kufanya hivyo licha ya uadui unaoibuliwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Iran kuishtaki "Google" kwa kupotosha jina la "Ghuba ya Uajemi"
May 15, 2025 00:35Kituo cha Kitaifa cha Anga za Juu cha Iran kimesema kitachukua hatua za kisheria dhidi ya kampuni ya Google ya Marekani na majukwaa mengine ya kimataifa kutokana na kupotoshwa kwa jina la kihistoria la Ghuba ya Uajemi.
-
Qalibaf ataka ushirikiano wa vikwazo dhidi ya Israel na kuundwa nchi huru ya Palestina
May 14, 2025 08:09Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezitaka nchi za Kiislamu kuuwekea vikwazo vya kisiasa, kiuchumi na kijeshi utawala wa Kizayuni wa Israel ili kukomesha mauaji ya kimbari huko Gaza.
-
IRGC yajibu vitisho vya US: Iran ipo tayari kwa senario yoyote
May 14, 2025 08:02Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema Iran iko tayari kwa hali yoyote ile, wakati huu ambapo Marekani inatoa vitisho vya kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya nchi hii, akisisitiza kwamba maadui watafedheheshwa wakijaribu kuingia katika makabiliano na Jamhuri ya Kiislamu.