-
Iran: Hakuna haja ya kuendelea na mazungumzo iwapo Marekani....
May 14, 2025 08:00Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi amesisitiza kuwa haki ya Jamhuri ya Kiislamu ya kurutubisha madini ya urani ni "mstari mwekundu" wa taifa hili, akisisitiza kuwa, kufikiwa makubaliano na Marekani kuhusu mpango wa amani wa nyuklia wa nchi hii kunategemea kufuata kanuni hizo.
-
Qalibaf: Umoja wa Mabunge ya Asia ni fursa ya kuendeleza uhusiano na nchi za Kiislamu
May 14, 2025 03:28Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amezungumzia umuhimu wa Umoja wa Mabunge ya Kiislamu kwa ajili ya kustawisha uhusiano kati ya nchi za Kiislamu na kusema: Kushiriki nchi 38 za Kiislamu katika mkutano wa 19 wa Mabunge ya Kiislamu ni fursa ya kuendeleza uhusiano kati ya nchi hizo.
-
Baqaei: Kusimamisha miradi ya nyuklia ya Iran kimsingi si jambo linalojadiliwa katika mazungumzo na Marekani
May 14, 2025 03:13Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa suala la kusimamisha miradi ya nyuklia ya Iran kimsingi halijadiliwi katika mazungumzo na Marekani na kwamba miradi yetu ya nyuklia bila shaka itaendelea kwa jadi.
-
Iran yailaani Israel kwa kupiga mabomu kambi za wakimbizi Palestina
May 13, 2025 23:17Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi ya hivi karibuni ya anga dhidi ya kambi za wakimbizi wa Kipalestina yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel na kusababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya Wapalestina wasio na hatia wakiwemo watoto wadogo.
-
Iran, Misri zataka kukomeshwa mashambulizi ya Israel huko Gaza
May 13, 2025 23:16Wanadiplomasia wakuu wa Iran na Misri wamesisitiza kuwa kuna haja ya kukomeshwa mashambulizi ya utawla wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Mkutano wa 31 wa Nyuklia wa Iran wafunguliwa mjini Mashhad
May 13, 2025 08:57Mkutano wa 31 wa Nyuklia wa Iran, ulioandaliwa na Jumuiya ya Nyuklia ya Iran na kuungwa mkono na Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI), umefunguliwa katika mji wa Mashhad, uliopo kaskazini-mashariki mwa Iran.
-
Iran kujiunga na safu ya watengenezaji wa ndege za kibiashara duniani
May 13, 2025 03:34Sambamba na maendeleo ya mradi wa uundaji wa ndege ya kwanza ya jet ya Iran ya kubeba abiria 8, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivi karibuni itajiunga na kundi dogo la watengenezaji wa ndege za kibiashara duniani.
-
Mauzo ya tende za Iran nje ya nchi yapindukia dola milioni 205 kwa mwaka
May 13, 2025 01:05Iran iliuza tende zenye thamani ya zaidi ya dola milioni 205 katika mwaka wa kalenda wa Kiirani wa 1403 (uliomalizika Machi 20, 2025), kwa mujibu wa taarifa mpya kutoka Mamlaka ya Forodha ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRICA), ikionyesha nafasi imara ya nchi hii katika soko la kimataifa la tende.
-
"Iran imeazimia kweli kufikia makubaliano katika mazungumzo ya nyuklia"
May 12, 2025 07:43Rais wa Iran amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu iko "jadi" katika mazungumzo yake yasiyo ya moja kwa moja na Marekani ili kufikia makubaliano yenye msingi wa amani, na kusisitiza azma ya Jamhuri ya Kiislamu ya kuendelea kutekeleza shughuli zake za amani za nyuklia.
-
Araqchi: Awamu ya nne wa mazungumzo na Marekani imekuwa makini zaidi kuliko nyingine
May 12, 2025 02:22Baada ya kumalizika duru ya nne ya mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana kati ya Iran na Marekani, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: "Mazungumzo hayo yalikuwa mazito zaidi, yenye umakini zaidi, yaliyo wazi zaidi na yanayoangalia mbele zaidi kuliko duru tatu zilizopita."