-
Kutekelezwa Makubaliano ya Kifedha kati ya Iran na Russia
Jan 20, 2025 23:03Gavana wa Benki Kuu ya Iran, Mohammadreza Farzin, amesema kuwa kupitia utekelezaji wa makubaliano ya kifedha kati ya Iran na Russia, sarafu za mataifa haya mawili zitakuwa msingi wa biashara kati ya nchi hizo kwa mujibu wa kiwango cha mabadilishano kilichokubaliwa sokoni.
-
Rais wa Iran awapongeza wananchi wa Gaza kwa ushindi dhidi ya Israel
Jan 20, 2025 07:57Rais Masoud Pezeshkian wa Iran leo Jumatatu amewapongeza wananchi wa Ukanda wa Gaza kwa ushindi wao katika kukabiliana na vita vya kikatili na mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel yaliyoendelea kwa miezi 15.
-
Kamanda wa Kikosi cha Quds: Kipigo kikubwa zaidi dhidi ya Israel kimeonekana
Jan 20, 2025 00:02Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) amesema kuwa, kuanza utekelezaji wa usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza kumedhihirisha pigo na kushindwa zaidi kwa utawala wa Kizayuni kutadhihirika.
-
Mazungumzo ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Yemen kuhusu matukio ya eneo
Jan 19, 2025 23:06Sayyid Abbas Araqchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amefanya mazungumzo ya simu na Jamal Ahmed Ali Amer, Waziri wa Mambo ya Nje na Wahamiaji wa Jamhuri ya Yemen, na kusisitiza kuendelea kwa msaada wa Iran kwa serikali na watu wa Yemen.
-
Kiongozi wa Mapinduzi atoa mkono wa pole kufuatia kuuawa shahidi Mahakimu wawili wa Idara ya Mahakama
Jan 19, 2025 07:11Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ametoa salamu za rambirambi na mkono wa pole kufuatia kuuawa shahidi katika shambulio la kigaidi mahakimu wawili wa Idara ya Mahakama ya Iran.
-
Pezeshkian: Hatuhitaji Magharibi kulinda usalama wa eneo hili
Jan 19, 2025 02:44Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Iran na Russia kwa kushirikiana vizuri zinaweza kufuata sera huru na kudhamini usalama wa kisiasa na kiuchumi wa eneo hili.
-
Mashauriano ya Iran na Ethiopia ya kupanua uhusiano wa kiuchumi
Jan 19, 2025 02:32Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya Bunge amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mshauri katika Wizara ya Masuala ya Kigeni ya Ethiopia ambapo wamejadiliana njia za kupanua ushirikiano wa kiuchumi baina ya nchi hizi mbili ikiwemo uanachama katika kundi la "BRICS".
-
Makubaliano ya ushirikiano wa kimkakati kati ya Iran na Russia; ni nini na kwa nini ni muhimu?
Jan 18, 2025 09:25Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Russia zimetiliana saini makubaliano ya ushirikiano wa kimkakati katika safari ya Rais Masoud Pezeshkian mjini Moscow.
-
Araqchi: Asili ya makubaliano ya Iran na Russia ni ya kiuchumi
Jan 18, 2025 07:37Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa makubaliano ya kina ya kimkakati ya ushirikiano kati ya Iran na Russia yanahusu vipengee vyote vya uhusiano wa nchi na kwamba asili ya makubaliano hayo zaidi ni katika uga wa uchumi.
-
Rais Pezeshkian arejea Tehran baada ya kutembelea Tajikistan na Russia
Jan 18, 2025 03:15Rais Masoud Peshkeskian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye alikuwa kwenye ziara za kikazi za kutembelea Dushanbe na Moscow akiongoza ujumbe wa ngazi za juu kwa mwaliko rasmi wa Marais Emomali Rahmon wa Tajikistan na Vladimir Putin wa Russia, amerejea hapa Tehran mapema leo Jumamosi.