-
Qalibaf: Iran imesimama imara kuwatetea Waislamu duniani
Jan 17, 2025 23:12Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema: Iran siku zote inasisima imara na imeonyesha kuwa ni nchi pekee inayowatetea Waislamu wote bila ya kujali madhehebu zao na imetoa maelfu ya mashahidi katika njia hii.
-
Rais Pezeshkian: Iran, Russia ziko imara katika uhusiano ‘nyeti wa kimkakati’
Jan 17, 2025 10:40Rais Masoud Pezeshkian anasema Iran na Russia zimesimama kidete katika uhusiano "nyeti, muhimu na wa kimkakati" wa pande zote.
-
Imamu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Ushindi wa Gaza ni muujiza wa kambi ya Muqawama
Jan 17, 2025 10:39Imamu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran ameutaja ushindi wa Wapalestina katika Ukanda wa Gaza dhidi ya utawala ghasibu wa Israel kuwa ni muujiza wa Muqawama.
-
Araqchi aipongeza Hamas kwa ushindi dhidi ya Israel
Jan 17, 2025 10:33Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameipongeza Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) kwa ushindi wa muqawama na wananchi wa Palestina dhidi ya Israel katika vita na mauaji ya kimbari ya utawala huo katika Ukanda wa Gaza.
-
Rais wa Iran awasili Russia kutia saini mkataba wa ushirikiano wa kistratijia wa miaka 20
Jan 17, 2025 09:37Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amewasili nchini Russia katika hatua ya pili ya ziara yake baada ya ziara yake ya siku mbili nchini Tajikistan.
-
Ghalibaf: Changamoto ya uhusiano wa kiuchumi wa Iran na Afrika ni usafiri
Jan 17, 2025 03:51Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameyataja matatizo ya usafiri kuwa ni miongoni mwa changamoto kubwa katika kupanua uhusiano wa kiuchumi wa Iran na bara la Afrika akisema: Uwezo wa kimataifa kama wa kundi la BRICS na Shanghai ni fursa muhimu za kustawisha ushirikiano wa kiuchumi.
-
Iran: Miezi 15 ya jinai za wavamizi huko Ghaza isingewezekana bila ya msaada wa Marekani na Magharibi
Jan 17, 2025 03:50Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetangaza kuwa, sambamba na kusitishwa mauaji ya kimbari huko Ghaza, jumuiya ya kimataifa inapaswa kukabiliana kwa umakini na ipasavyo uasi wa utawala wa Kizayuni katika eneo lote la Palestina inayokaliwa kwa mabavu. Inabidi kuandaliwe pia uwanja wa kukamatwa, kufunguliwa mashtaka na kuadhibiwa viongozi magaidi wa utawala katili wa Israel kwa jinai za kivita.
-
Spika wa Bunge la Iran awasili Ethiopia kwa ziara rasmi
Jan 16, 2025 23:50Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amewasili Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia akiongoza ujumbe wa ngazi za juu Bunge kwa mwaliko wa Spika wa Baraza la Wawakilishi la Ethiopia.
-
Rais Pezeshkian: Tajikistan ni mshirika wa kimkakati wa Iran katika eneo
Jan 16, 2025 23:45Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Tajikistan ni miongoni mwa washirika wetu wa kistratijia katika eneo hili, na kuna uhusiano wa karibu wa ujirani baina ya nchi hizi mbili.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Muqawama wa Palestina umeilazimisha Israel kurudi nyuma
Jan 16, 2025 07:47Baada ya kutangazwa makubaliano ya usitishaji vita huko Gaza, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Imam Ali Khamenei ametuma ujumbe kwenye mitandao ya kijamii na kuandika: Subira na kusimama kidete kwa wananchi na Muqawama wa Wapalestina vimeulazimisha utawala wa Kizayuni kurudi nyuma.