-
Rais Pezeshkian: Hiki ni kiduchu tu cha uwezo wetu, Netanyahu usicheze na Iran
Oct 02, 2024 00:14Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Daktari Masoud Pezeshkian amesema "Jibu madhubuti limetolewa kwa uchokozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kwamba jibu hilo ni sehemu ndogo sana ya uwezo wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran: Bendera ya Hizbullah na Muqawama haitaanguka chini
Oct 01, 2024 10:27Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran amesisitiza kuwa bendera ya Hizbullah na Muqawama kamwe haitoanguka chini na amesisitiza kuwa, utawala ghasibu wa Kizayuni na Marekani watenda jinai wafahamu kwamba, hivi sasa Iran itaunga mkono zaidi kambi ya Muqawama kuliko ilivyokuwa huko nyuma.
-
Rais wa Iran kuelekea Qatar kesho Jumatano
Oct 01, 2024 10:23Rais wa Iran kesho Jumatano ataondoka hapa Tehran na kuelekea Qatar kwa madhumuni ya kushiriki katika kikao rasmi cha nchi mbili na kushiriki katika Jukwaa la Mazungumzo ya Ushirikiano wa Asia.
-
Kukosoa Araghchi "kutochukua hatua" Baraza la Usalama kukabiliana na jinai za Wazayuni dhidi ya Gaza na Lebanon
Oct 01, 2024 05:01Sayyid Abbas Araghchi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameitaja hatua ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ya kutochukua hatua kutokana na ukwamishaji mambo wa Marekani na waungaji mkono wengine wa Magharibi wa Israel kuwa ndio sababu kuu ya kuendelea jinai, chokochoko na vitendo visivyo halali vya utawala haramu wa Kizayuni.
-
Rais wa Iran akosoa undumakuwili wa Marekani na Ulaya kuhusu haki za binadamu
Sep 30, 2024 22:49Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa undumakuwili wa Marekani na madola ya Ulaya kuuhusiana na haki za binadamuu na kusema, kimya cha nchi za magharibi mbele ya mauaji ya maelfu ya watu wasio na hatia ni kugonga muhuri wa kuunga mkono jinai hizi.
-
Rais Pezeshkian: Damu ya shahidi Nasrullah itaendelea kuchemka na itasimama wima mbele ya dhulma
Sep 30, 2024 11:09Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani na waungaji mkono wa utawala wa Kizayuni wamewaonyesha walimwengu jinsi haki za binadamu, utu wa binadamu na sheria za kimataifa zinavyokiukwa, magaidi na wahalifu wanaitwa watetezi wa haki za binadamu na waungaji mkono wa haki za binadamu kwa wanaodhulumiwa na wanaitwa kuwa ni magaidi.
-
Abu Sharif: Irada ya muqawama ina nguvu kuliko njama yoyote
Sep 30, 2024 08:31Mwakilishi wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina amesema baada ya utawalal wa Kizayuni kumuua shahidi Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon kwamba: Licha ya kuipoteza nembo hiyo adhimu, lakini si tu muqawama hautadhoofishwa bali utaendeleza njia yake kwa nguvu zaidi na kwa azma kamili.
-
Subirini; jibu la kamanda wa jeshi la Iran kuhusu radiamali ya Tehran kwa mauaji ya shahidi Nasrullah
Sep 30, 2024 07:49Kamanda mkuu wa jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuhusu radiamali ya Iran na mhimili wa muqawama kwa mauaji ya Sayyid Hassan Nasrullah kuwa, subirini.
-
Tume ya Haki za Binadamu ya Iran yatoa taarifa kulaani jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Lebanon
Sep 30, 2024 07:44Tume ya Haki za Binadamu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ikilaani shambulio la kigaidi la utawala katili na unaotenda jinai wa Kizayuni katika eneo la Dhahiya kusini mwa Beirut, mji mkuu wa Lebanon lililowauwa shahidi shakhsia watajika wa muqawama pamoja na mujahid Sayyid Hassan Nasrullah Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Rais Pezeshkian: Jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel hazitabaki bila kujibiwa
Sep 30, 2024 04:39Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema ni lazima Tehran itoe jibu kwa utawala unaotenda jinai wa Israel.