-
Rekodi mpya katika uzalishaji wa umeme wa nyuklia nchini Iran
Sep 30, 2024 04:32Kiwanda pekee cha nishati ya nyuklia cha Iran kilifikia kiwango cha uzalishaji cha zaidi ya saa bilioni 7 za kilowati katika mwaka huu wa Hijria Shamsiya.
-
Kamanda Qaani: Tutakuwa bega kwa bega na Hizbullah hadi Quds na Palestina zitakapokombolewa
Sep 30, 2024 00:00Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema, Iran itakuwa bega kwa bega na harakati ya Muqawama ya Lebanon ya Hizbullah hadi ukombozi wa Palestina na Quds Tukufu.
-
Utayarifu na uwezo wa Iran wa kukabiliana na migogoro inayoibuliwa na utawala wa Kizayuni na Marekani
Sep 29, 2024 08:29Sayyid Abbas Araghchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, katika kikao na Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ametoa onyo kali kuhusu hatua za utawala wa Kizayuni na Marekani za kuibua migogoro mipya katika eneo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Baraza la Usalama linapaswa kuchukua hatua kukomesha jinai za Israel
Sep 29, 2024 07:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa heshima na hadhi ya Umoja wa Mataifa imeharibiwa vibaya isipokuwa kama Baraza la Usalama litachukua hatua za haraka kukomesha uchokozi wa utawala ghasibu wa Israel.
-
SEPAH: Malengo matukufu ya ukombozi wa Quds yamekaribia kufikiwa
Sep 29, 2024 02:40Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) ametoa ujumbe maalumu wa pongezi na wa mkono wa pole kufuatia kuuawa shahidi Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon na kusisitiza kuwa, malengo matukufu ya ukombozi wa Quds yamekaribia kufikiwa na historia itathibitisha hilo.
-
Ghalibaf: Sayyid Hassan Nasrullahh ameuawa shahidi katika njia ya ukombozi wa Quds
Sep 29, 2024 02:40Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon ameuawa shahidi katika njia takatifu ya kuupigania Uislamu na ukombozi wa Quds.
-
Iran yazitaka nchi za Kiislamu kuungana kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni
Sep 29, 2024 02:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa nchi za Kiislamu zina wajibu wa kuungana na kushikamana katika kukabiliana na jinai za utawala wa Kizayuni huko Palestina na Lebanon.
-
Ayatullah Khamenei: Vipigo vya Muqawama dhidi ya utawala unaozidi kunyauka wa Kizayuni vitakuwa shadidi
Sep 28, 2024 22:47Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe kwa mnasaba wa kuuawa shahidi Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon, akisisitiza kuwa: Njia ya mapambano ya Sayyid wa Muqawama itaendelea na mashambulizi ya Kambi ya Muqawama yatakuwa shadidi zaidi kwenye kiwiliwili kilichochakaa na kinachoeleka kuangamia cha utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Rais Pezeshkian: Kuuawa shahidi Sayyid Nasrullah kunaimarisha zaidi Muqawama
Sep 28, 2024 12:11Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuuawa shahidi watu mashuhuri wa Kambi ya Muqawama, akiwemo kiongozi wa Hizbullah, Sayyid Hassan Nasrullah, kunaimarisha zaidi mti wa mwema wa Muqawama na mapambano, na kuongeza kuwa: "Ulimwengu hautasahau kwamba amri ya shambulio hilo la kigaidi imetolewa New York."
-
Ombi la Iran kwa BRICS
Sep 28, 2024 08:02Kuacha kutumia sarafu ya dola, kukabiliana na vikwazo vya upande mmoja vya nchi za Magharibi, kuwa na sekretarieti ndogo na ya haraka na kufanyika vikao vya BRICS katika nchi wanachama kwa mujibu wa hali ya kijiografia, ni matakwa manne yaliyowasilishwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kikao cha Mawaziri wa Mambo ya Nje wa kundi la BRICS pambizoni mwa Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York.