-
Iran: Mkuu wa vyombo vya habari wa Hizbullah aliyeuawa shahidi alikuwa "sauti nzito" ya Lebanon
Nov 18, 2024 09:20Iran imelaani vikali mauaji ya msemaji wa Hizbullah Mohammad Afif katika shambulio la Israel lililolenga jengo moja katikati mwa Beirut, na kusema Shahidi Afif alikkuwa 'sauti nzito," ya taifa la Lebanon.
-
Takhte Ravanchi: Sera za mashinikizo ya juu zaidi dhidi ya Iran zitafeli
Nov 18, 2024 09:12Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesisitiza kuwa jitihada zote za kuiwekea Tehran mashinikizo ya juu zaidi zitafeli.
-
Araghchi: Uwekaji vikwazo wa Ulaya dhidi ya Iran hauna msingi wa kisheria, kimantiki wala kimaadili
Nov 18, 2024 04:14Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araqchi ametoa mjibizo kwa uamuzi wa Umoja wa Ulaya wa kutaka kuyawekea vikwazo mashirika ya vyombo vya majini ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kueleza kwamba hatua hiyo ya Ulaya haina msingi wowote wa kisheria, kimantiki wala kimaadili.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran: Tutaendelea kuunga mkono Mhimili wa Muqawama
Nov 18, 2024 03:54Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Tehran itaendelea kuuunga mkono Mhimili wa Muqawama, serikali na wananchi wa Syria.
-
Maulamaa wa Kisunni Iran wawaandikia barua wenzao katika Ulimwengu wa Kiislamu kuhusu Vita vya Ghaza
Nov 17, 2024 10:39Mamia ya Maulamaa mashuhuri wa Kisunni wa nchini Iran wametoa wito wa kuchukuliwa hatua za kivitendo na Maulamaa wa Ulimwengu wa Kiislamu katika kukabiliana na jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Araghchi: Wamagharibi wameonyesha nia ya kuanza tena mazungumzo ya nyuklia
Nov 17, 2024 04:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi, amesema kuwa hivi sasa nchi za Ulaya zinaonyesha nia ya kuanza tena mazungumzo ya nyuklia na kueleza kuwa: Yumkini mazungumzo hayo yakafanya hivi karibuni.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran akutana na mwenzake wa Syria
Nov 17, 2024 04:05Waziri wa Ulinzi wa Iran, Brigedia Jenerali Azizi Nasirzadeh, ambaye yuko ziarani nchini Syria, amekutana na na kufanya mazungumzo na waziri mwenzake leo Jumapili.
-
Baghaei: Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa hajakutana na Elon Musk
Nov 16, 2024 22:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baghaei amekanusha habari za kufanyika mkutano kati ya mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa na mshauri wa Rais mpya wa Marekani, Elon Musk.
-
Indhari ya Iran kuhusu mchezo wa kisiasa wa Troika ya Ulaya
Nov 16, 2024 22:56Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika mazungumzo na Rafael Grossi Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa KImataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) hapa Tehran kuwa: "Kile ambacho Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inakitaka katika teknolojia ya nyuklia kinakwenda sambamba kikamilifu na mifumo na vibali vya kisheria vya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki."
-
Iran yalitaka Baraza la Usalama kuchukua hatua za kukomesha jinai za Israel
Nov 16, 2024 09:03Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ametoa mwito wa kuchukuliwa hatua za lazima ili kukomesha jinai za utawala ghasibu wa Israel.