-
Kamanda: Iran inaona fakhari kumiliki makombora yanayopiga kilomita 2000
Sep 26, 2024 00:28Kamanda wa Jeshi la Anga la Iran alisema amesema jeshi la Jamhuri ya Kiislamu linajivunia makombora yenye uwezo wa kupiga shabaha kwa usahihi mkubwa, umbali wa zaidi ya kilomita 2000.
-
Kiongozi Muadhamu: Wanamuqawama wa Palestina na Hizbullah ya Lebanon ndio washindi
Sep 25, 2024 10:30Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameonana na wanaharakati wa Vita vya Kujihami Kutakatifu na Muqawama na kusisitiza kuwa, kambi ya Muqawama ya Palestina na Hizbullah ya Lebanon ndiye mshindi.
-
Sisitizo la Rais Pezeshkian katika Baraza Kuu la UN kuhusu vipaumbele vya sera za nje za Iran
Sep 25, 2024 08:47Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran jana Jumanne alihutubia Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) mjini New York kuhusu vipaumbele vikuu vya sera za nje za Iran kuhusiana na matukio ya kikanda na kimataifa.
-
Tehran yakadhibisha tuhuma za maafisa wa Sweden dhidi ya Iran
Sep 25, 2024 04:26Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Sweden umekadhibisha tuhuma zisizo na msingi na za uongo zilizotolewa na maafisa wa serikali ya Sweden dhidi ya Tehran.
-
Rais Pezeshkian: Umwagaji damu za maelfu ya watu wasio na hatia Lebanon hautabaki bila majibu
Sep 25, 2024 00:07Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, jinai za kiholela na za kigaidi zilizofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika siku zilizopita na uchokozi wake mkubwa dhidi ya Lebanon ambao umemwaga damu za maelfu ya watu wasio na hatia hautabaki bila majibu.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu ataka kusitishwa mauaji ya halaiki ya utawala wa Kizayuni
Sep 24, 2024 23:03Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu amelaani jinai za hivi karibuni za utawala wa Kizayuni huko Lebanon na kutaka kuwepo na uungaji mkono wa nchi za Kiislamu na serikali zinazotetea amani na usalama duniani kwa ajili ya kusitisha mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel.
-
Tathmini ya hotuba ya Rais wa Iran katika mkutano wa kuimarisha malengo ya Umoja wa Mataifa
Sep 24, 2024 08:23Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefafanua mitazamo ya Iran kuhusu 'Mkataba wa Mustakabali wa Kuimarisha Malengo ya Umoja wa Mataifa.
-
Rais Pezeshkian: Iran haijawahi katu kuwa na nia ya kumiliki silaha za nyuklia
Sep 24, 2024 07:45Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Iran amesema, Iran haijawahi katu kuwa na nia ya kumiliki silaha za nyuklia, bali imeheshimu na kutekeleza ahadi zake kulingana na makubaliano ya kimataifa ya JCPOA.
-
Rais Pezeshkian atilia mkazo kuimairishwa uhusiano wa kiusalama baina ya Iran na Uturuki
Sep 24, 2024 04:02Rais Masoud Pezeshkian amefanya mazungumzo na Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki na kusisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kuimarisha uhusiano wake wa pande zote na Uturuki yakiwemo masuala ya usalama.
-
Mohsen Rezai: Kisasi cha damu ya Ismail Haniyeh kinakuja
Sep 24, 2024 04:01Mjumbe wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumzia jinai ya utawala wa Kizayuni ya kumuua kigaidi Ismail Haniyeh, Mkuu wa zamani wa Ofisi ya Kisiasa ya HAMAS hapa Tehran na kusisitiza kuwa, kisasi cha damu ya mwanamapambano huyo wa Palestina, kinakuja.