-
Balozi wa Iran UN: Maghala ya nyuklia ya Israel ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia
Sep 05, 2024 07:13Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema, silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni wa Israel ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa kikanda na wa ulimwengu mzima.
-
Muirani Mehrzad, mwanaume wa pili kwa urefu zaidi duniani, analala sakafuni katika Kijiji cha Olimpiki, Paris
Sep 05, 2024 07:10Mwanaume wa pili kwa urefu zaidi duniani, Morteza Mehrzad Selakjani ambaye ni raia wa Iran, analazimika kulala chini sakafuni katika Kijiji cha Olympic mjini Paris anakoshiriki michuano ya Olimpiki ya Walemavu inayoendelea sasa nchini Ufaransa.
-
Iran: Mustakbali bora wa Ulimwengu wa Kiislamu ndiyo sababu ya kuimarishwa uhusiano wetu na Saudia
Sep 05, 2024 02:34Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Riyadh amesema kwa mnasaba wa kutimia mwaka mmoja tangu nchi mbili za Iran na Saudia zirejeshe uhusiano wao wa kidiplomasia kwamba, lengo la Tehran katika kuimarisha uhusiano wake na Saudi Arabia ni kuyaletea manufaa mataifa haya mawili ya Kiislamu na kuuandalia umma wa Kiislamu mustakbali bora.
-
Naibu Kamanda wa IRGC: Jibu la Iran kwa mauaji ya Haniyeh litakuwa 'tofauti, la kushangaza' na la wakati muafaka'
Sep 04, 2024 23:03Naibu Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) ameonya kuwa jibu la Tehran kwa mauaji ya Ismail Haniyeh, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Hamas aliyeuawa kigaidi mjini Tehran, litakuwa tofauti na la kushangaza.
-
Azma ya Iran na Russia ya kukamilisha hati jumuishi ya ushirikiano
Sep 04, 2024 23:00Akikaribisha matamshi ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusu kuendelea uhusiano na Russia, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia amesema: Hati ya makubaliano jumuishi ya ushirikiano kati ya tehran na Moscow itakamilika katika siku chache za usoni.
-
Kan'ani: Sauti ya kuvunjika mifupa ya Uzayuni inasikika zaidi
Sep 04, 2024 11:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: Kuendelea kuwepo utawala wa Kizayuni wa Israel kunaelekea ukingoni, na bila shaka, mhalifu wa kivita kama Netanyahu anaharakisha kuporomoka kwa utawala huo ndani na kimataifa kwa kuendelea kusalia madarakani.
-
Kuunga mkono Iran maamuzi ya wananchi na muqawama wa Palestina
Sep 04, 2024 09:11Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza kuwa, Tehran inaunga mkono makubaliano na uamuzi wowote wa makundi ya muqawama na wananchi wa Palestina.
-
Kan'ani: Wahalifu wa Tel Aviv ni wafyonza damu
Sep 04, 2024 03:53Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameashiria mauaji ya muigizaji maarufu wa Kipalestina yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel na kusema kuwa, damu ya Rashad abu Skheileh na zaidi ya Wapalestina wengine 40,000 wa Ukanda wa Gaza ni ithibati ya roho chafu na ya kikatili ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Wairan waghariki katika kumbukizi ya kuuawa shahidi Imam Ridha AS
Sep 04, 2024 03:32Wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran tokea jana usiku wamezama katika maombolezo ya kukumbuka kuuawa shahidi Imam Ali Ridha (AS), mjukuu wa Mtume Mtukufu (SAW) miaka 1242 iliyopita.
-
Iran yawaita mabalozi wa UK, Australia mjini Tehran
Sep 04, 2024 03:30Balozi wa Uingereza mjini Tehran ameitwa katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran na kukabidhiwa malalamiko ya Jamhuri ya Kiislamu, baada ya serikali ya London kuwawekea vikwazo shakhsia watatu Wairan na taasisi moja ya Iran.