-
Araqchi: Ukosefu wa usalama katika Ghuba ya Uajemi ni matokeo ya uchokozi wa adui
Mar 25, 2026 07:59Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China wamezungumza kwa simu na kujadili matukio ya hivi sasa kuhusiana na Vita vya Ramadhani.
-
Umeme wakatwa kaskazini mwa Tel Aviv kufuatia mashambulizi ya makombora ya Iran
Mar 25, 2026 07:39Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimeripoti kuwa huduma ya umeme imekatwa katika moja ya miji ya kistratejia ya kaskazini mwa Israel kufuatia mashambulizi ya makombora ya Iran.
-
Makombora ya Iran yalenga Kamandi ya Kijeshi ya Israel na Manoari na Marekani ya Abraham Lincoln
Mar 25, 2026 06:35Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeilenga kamandi ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni iliyoko katika eneo la kaskazini la Safed katika wimbi jipya la mashambulizi ya makombora.
-
Jenerali Abdollahi: Jeshi la Iran litaendeleza mapambano ya kujihami hadi ushindi kamili
Mar 25, 2026 05:54Kamanda wa Kamandi ya Khatam al‑Anbiya (SAW) katika Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika ujumbe wake kwamba: “Vikosi vyenye nguvu vya ulinzi vya Iran ya Kiislamu, kwa utiifu kamili kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, vimesimama imara katika ahadi yao ya kulinda taifa tukufu na lenye ushindi la Iran, na vitaendeleza njia hii tukufu kwa msaada wa watu wenye ufahamu na ushujaa wa Iran ya Kiislamu hadi ushindi kamili.”
-
Msemaji wa Jeshi la Iran: Msiite kushindwa kuwa ni makubaliano
Mar 25, 2026 04:57Msemaji wa Kamandi ya Khatamul Anbiya (SAW) ya Jeshi la Iran amewahutubu watawala wa Marekani na kuwaambia kuwa, wasiite kushindwa kuwa ni makubaliano.
-
Marais wa Iran na Ufaransa wazungumza kuhusu kupunguza mvutano Asia Magharibi
Mar 25, 2026 04:25Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesema kuwa katika mazungumzo ya simu na Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, walijadili suala la Lango Bahari la Hormuz na namna ya kupunguza mvutano katika eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati).
-
Rais Pezeshkian: Ukosefu wa usalama Lango la Hormuz ni matokeo ya mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran
Mar 24, 2026 07:53Rais Masoud Pezeshhkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif ambapo pande hizo mbili zimejadili uhusiano wa nchi mbili, matukio ya sasa katika kanda ya Magharibi mwa Asia na athari za vita haramu vya Marekani na utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Iran kwa usalama na kanda na dunia nzima.
-
Brigedia Jenerali Rezaei amwambia Trump: Ukipiga miondombinu yetu hatutalipiza kisasi cha jicho kwa jicho, bali kichwa kwa jicho
Mar 24, 2026 07:52Kamanda wa zamani wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesisitiza udharura wa kuendelezwa vita hadi Iran itakapolipwa gharama kamili za hasara zilizosababishwa na adui Mmarekani na Mzayuni.
-
Jeshi la Iran: Droni za adui zilizotunguliwa hadi sasa ni 132
Mar 24, 2026 06:49Idara ya Uhusiano wa Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) imetangaza kuangushwa kwa ndege isiyo na rubani au droni moja ya kivita aina ya Hermes ya utawala haramu wa Israel katika anga ya Tehran mapema Jumanne.
-
Majibu ya Qalibaf kwa madai ya uongo ya Trump: Watu wa Iran wanataka wavamizi waadhibiwe kikamilifu
Mar 24, 2026 05:14Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amejibu madai ya uongo ya rais Donald Trump wa Marekani kuhusu kuwepo kwa mazungumzo na Iran.