-
Mamilioni wamiminika mitaani Iran kuadhimisha ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Feb 11, 2026 03:38Mamilioni ya wananchi kutoka matabaka yote ya kijamii wamejitokeza mitaani kote nchini Iran kushiriki maandamano ya kitaifa yanayoashiria maadhimisho ya miaka 47 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Iran yaonya kuhusu njama za Israel huku ikiendeleza mazungumzo ya kidiplomasia na Marekani
Feb 10, 2026 23:37Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ametoa tahadhari kuhusu azma ya utawala wa Israel ya kuishawishi Marekani iingie katika vita vingine dhidi ya Iran, wakati mazungumzo mapya ya nyuklia kati ya Tehran na Washington yakiwa yameanza.
-
Maadhimisho ya Mapinduzi ya Kiislamu: Maandamano kufanyika katika miji 1,400, waandishi habari 7,700 wanaakisi tukio hilo
Feb 10, 2026 11:41Sherehe na maandamano ya kuadhimisha miaka 47 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yatafanyika katika miji zaidi ya 1,400 nchini kote, huku waandishi wa habari wa ndani na nje wapatao 7,700 wakitarajiwa kuripoti matukio hayo.
-
Larijani akutana na Sultani wa Oman, mazungumzo baina ya wawili yaendelea kwa saa tatu
Feb 10, 2026 10:48Akiendelea na mashauriano yake ya kikanda, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili Muscat mapema leo akiongoza ujumbe wa ngazi za juu na kufanya mazungumzo na Mfalme Haitham bin Tariq katika mkutano ulioendelea kwa karibu saa tatu.
-
Rais Pezeshkian: Iran haitaki vita; mashinikizo ya kiuchumi yanalenga kuichafua serikali
Feb 10, 2026 03:52Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza tena msimamo wa Iran wa kuunga mkono amani, akisema kuwa nchi hii haijawahi kutaka kuanzisha vita, licha ya kukabiliwa na uhasama wa wazi kutoka kwa maadui zake.
-
Iran inaweza kupunguza kiwango cha urutubishaji urani iwapo ‘vikwazo vyote vitaondolewa’
Feb 10, 2026 03:46Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) amesema kuwa uwezekano wowote wa kupunguza kiwango cha urutubishaji wa urani ambayo sasa ni imefika hadi asilimia 60 utategemea kikamilifu iwapo vikwazo vyote dhidi ya nchi hiyo vitaondolewa.
-
Msemaji wa Majeshi: Iran haitasalimu amri mbele ya mashinikizo ya Marekani wakati wa mazungumzo
Feb 10, 2026 03:42Iran haitasalimu amri wala kukubali mashinikizo au masharti ya Marekani huku ikiendelea na mazungumzo na Washington, amesema Brigedia Jenerali Abolfazl Shekarchi, msemaji wa Vikosi vya Ulinzi vya Iran, katika mahojiano maalum na Press TV.
-
Rais Pezeshkian: Mazungumzo ya Iran na Marekani ni ‘fursa nzuri’ ya kutatua suala la nyuklia
Feb 09, 2026 22:57Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kuwa mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Marekani na Iran yanatoa fursa nzuri ya kufikia suluhu “inayoridhisha pande zote ” kuhusu suala la nyuklia la Iran.
-
Kiongozi Muadhamu awataka Wairani kuwakatisha tamaa maadui Bahman 22
Feb 09, 2026 07:20Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ametoa wito kwa taifa la Iran kuonyesha irada, azma thabiti na kusimama kidete, kwa kushiriki kwa wingi katika matembezi na mijumuiko ya kuadhimisha miaka 47 ya Mapinduzi ya Kiislamu, akisema kuwa umoja huo utamkatisha tamaa adui wa nchi hii.
-
Spika: Iran inajiimarisha kijeshi sambamba na diplomasia
Feb 09, 2026 06:41Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran), Mohammad-Bagher Ghalibaf amesema Jamhuri ya Kiislamu inafuatilia diplomasia sanjari na kuimarisha uwezo wake wa kiulinzi na kijeshi ili iweze kukabiliana na maadui zake.