-
Jeshi la Iran: Vidole vyetu viko kwenye kitufe cha kufyatua risasi, lakini hatutaki kuanzisha vita
Feb 09, 2026 03:25Mkuu wa vikosi vya Ulinzi vya Iran, Meja Jenerali Abdolrahim Mousavi, na Kamanda wa Jeshi la Iran, Meja Jenerali Amir Hatami, wamesisitiza kuwa, Iran haitafuti kuanzisha vita vya kikanda licha ya utayari wake kamili.
-
Pezeshkian: Iran haikubali mabavu na mantiki yake ya nyuklia imejikita katika Mkataba wa NPT
Feb 08, 2026 23:31Rais Masoud Pezeshkian amepongeza duru mpya ya mazungumzo ya nyuklia yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani na kuitaja kuwa “hatua ya kusonga mbele,” akisisitiza kuwa msimamo wa Tehran kuhusu suala hilo unategemea haki zilizoainishwa ndani ya Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT).
-
Jenerali Mousavi: Iran iko tayari kikamilifu kutoa jibu la haraka na kali kwa uchokozi wowote
Feb 08, 2026 23:30Mkuu wa Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa ingawa Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kikamilifu kutoa jibu la haraka, kali na litakaloleta majuto kwa uchokozi wowote, haina nia ya kuanzisha vita vya kikanda.
-
Uwezo wa kiuchumi wa Iran wa kushiriki katika masoko yanayoinukia
Feb 08, 2026 05:53Waziri wa Masuala ya Uchumi na Fedha wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili Riyadh, mji mkuu wa Saudi Arabia, kwa ajili ya kushiriki katika mkutano wa pili wa masoko yanayoinukia.
-
Iran kuokoa dola milioni 30 kwa kujizalishia aina 63 za dawa
Feb 08, 2026 05:44Iran imezindua bidhaa mpya 63 za dawa zinazozalishwa ndani ya nchi—ikiwa ni pamoja na fomula 19 zinazozalishwa kwa mara ya kwanza hapa nchini—hatua inayotarajiwa kuifanya nchi hiyi iokoe kati ya dola milioni 25 na 30 kila mwaka kwa fedha muhimu za kigeni, kwa kupunguza utegemezi wa dawa na malighafi zinazoagizwa kutoka nje.
-
Araqchi: Iran haiogopi kutumwa wanajeshi wa upande mwingine katika kanda hii
Feb 08, 2026 05:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kwamba Jamhuri ya Kiislamu haiogopi vitisho vya kijeshi, akisema: "Iran ni nchi nchi inayofuata diplomasia na mantiki, na wakati huo huo iko tayari kujilinda ili upande wowote usithubutu kulazimisha vita dhidi ya taifa la Iran."
-
Iran yasisitiza kuwa itavishambulia vituo vya kijeshi vya Marekani, si ardhi za nchi jirani
Feb 08, 2026 02:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi ameonya kwamba, iwapo Marekani itaishambulia Iran, vituo vya kijeshi vya nchi hiyo katika eneo la Asia Magharibi navyo vitashambuliwa.
-
Gaidi aliyefunzwa na Mossad kuendesha 'vita vya mitaani' aangamizwa na vikosi vya intelijensia vya Iran
Feb 08, 2026 02:49Sadeq Ashtari, kiongozi wa genge la kigaidi aliyepewa mafunzo na shirika la ujasusi la utawala wa kizayuni wa Israel Mossad kwa ajili ya kuendesha "vita vya mitaani" ameangamizwa katika mapigano na vikosi vya intelijensia vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Hatutafanya mazungumzo kuhusu makombora yetu, si sasa wala baadaye
Feb 07, 2026 23:18Sayyid Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesisitiza kwamba Iran haitafanya mazungumzo kuhusu makombora yake, kwa sababu maudhui hiyo inahusu masuala ya ulinzi tu.
-
Waziri wa Fedha wa US akiri hadharani: Tulisababisha uhaba wa dola ndani ya Iran ili kuchochea machafuko
Feb 07, 2026 23:00Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Kenneth Homer Bessent amekiri kuwa, Washington ilisababisha uhaba wa sarafu ya dola ya nchi hiyo ndani ya Iran, hatua ambayo ilisababisha kushuka kwa kasi kwa thamani ya sarafu ya Iran ya riali na kuibua mashinikizo ya kiuchumi yaliyochochea machafuko ya Desemba mwaka jana.