-
Iran yaishukuru Pakistan kwa kuwa pamoja nayo wakati wa vita vya kulazimishwa
Nov 26, 2025 03:03Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Kitaifa la Iran (SNSC) Ali Larijani ameishukuru Pakistan kwa kuiunga mkono Tehran wakati wa "vita visivyo vya haki" vya mwezi Juni 2025 vilivyoanzishwa na utawala wa Kizayuni na Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Larijani: Ushirikiano wa Iran na Pakistan unachangia amani ya kikanda
Nov 25, 2025 11:00Ali Larijani, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC), amesema ushirikiano kati ya Tehran na Islamabad katika nyanja mbalimbali unaimarisha amani na utulivu wa kieneo, na kuangazia nafasi muhimu ya Pakistan katika uwanja huo.
-
Mohsein Rezaei: Israel inaharakisha anguko lake kwa kuwauwa makamanda wa Muqawama
Nov 24, 2025 15:23Kamanda Mkuu wa zamani wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ameonya kuwa mauaji yanayofanywa na utawala wa Israel dhidi ya makamanda wa Muqawama yanaharakisha kuangamia utawala huo.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Oman wafanya mazungumzo mjini Muscat
Nov 24, 2025 07:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Seyed Abbas Araghchi amekutana na kufanya mazungumzo na mwenzake wa Oman Badr Al-Busaidi mjini Muscat Jumapili jioni na kujadili masuala mbalimbai yakiwemo ya uhusiano wa pande mbili na matukio muhimu ya kikanda.
-
Danny Citrinowicz: Ushawishi wa vyombo vya habari vya Iran barani Afrika umeongezeka
Nov 24, 2025 07:14Mtafiti mkuu wa Mpango wa Iran katika Taasisi ya Utafiti wa Usalama wa Taifa ya Israel (INSS) ameeleza wasiwasi wake kuhusu mwenendo wa ushawishi wa vyombo vya habari vya Iran barani Afrika na matokeo yake ya muda mrefu dhidi ya maslahi ya utawala wa Kizayuni barani humo.
-
Tehran: Azimio la IAEA dhidi ya Iran ni 'doa la fedheha' kwa watayarishaji wake
Nov 24, 2025 03:21Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani azimio lililopitishwa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kuhusu mpango wa amani wa nyuklia wa Tehran na kulitaja kuwa "doa la fedheha" kwa wafadhili wa azimio hilo.
-
Iran yaidhinisha miradi ya uwekezaji wa kigeni ya dola milioni 485
Nov 24, 2025 03:03Bodi ya uwekezaji wa kigeni ya Iran imeidhinisha maombi 67 yenye thamani ya dola milioni 485 wakati wa mkutano wake wa tisa wa mwaka, kuashiria maslahi mapya kutoka kwa wawekezaji wa kimataifa katika sekta nyingi.
-
Iran: Utawala wa kizayuni hauna mpaka katika kutenda jinai
Nov 23, 2025 12:06Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, utawala haramu wa Israel hauna mpaka katika kutenda jinai na wqala hauheshimu ahadi wala sheria yoyote ya kimataifa.
-
Kamanda: Jeshi la Iran liko tayari kukabiliana na tishio lolote
Nov 23, 2025 03:12Kamanda wa Jeshi la Nchi Kavu la Iran, akizungumza mbele ya makamanda wenzake, amesisitiza kuwa kwa kuzingatia maelekezo ya Kiongozi Muadhamu na kwa kutumia tajiriba ya vita vya zamani, hususan vita vya kulazimishwa vya siku 12 vya mwezi Juni, jeshi limeweka mkakati wa kuzingatia nguzo tano: utii wa uongozi, uadilifu, ufanisi, teknolojia na uboreshaji wa ujuzi.
-
Madini ya risasi na zinki yaimarisha hadhi ya Iran kama ngome ya madini Asia Magharibi
Nov 23, 2025 03:07Tarehe 22 Novemba, huadhimishwa kitaifa nchini Iran kama Siku ya Madini ya Risasi na Zinki ikiwa ni kuashiria nafasi kuu ya sekta hii na uhusiano wake wa karibu na malengo ya kiuchumi ya taifa.