-
Iran yapinga na kuyatoa maanani madai ya kundi la G7 dhidi yake
Nov 13, 2025 23:52Esmail Baghaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, madai yaliyomo kwenye taarifa iliyotolewa mwishoni mwa mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi zinazounda G7 uliofanyika nchini Canada kuhusu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hayana msingi wala nadhari na hayakubaliki.
-
Iran yasambaratisha mtandao wa mamluki wa Marekani na Israel
Nov 13, 2025 03:51Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran SEPAH kimesambaratisha mtandao wa kijasusi hapa nchini uliokuwa ukiendesha harakati za kuvuruga usalama na amani.
-
Aragchi: UN ichukue hatua baada ya Trump kukiri jukumu katika mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran
Nov 12, 2025 23:34Katika barua rasmi kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran Abbas Araghchi amelaani Marekani kwa jukumu lake katika kuunga mkono uchokozi wa kijeshi wa Israeli dhidi ya Iran mnamo Juni, kufuatia kauli za Rais Donald Trump akithibitisha usimamizi wa Marekani juu ya mashambulizi hayo.
-
Larijani: Hakuna ujumbe mpya uliotumwa Marekani
Nov 12, 2025 04:08Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amepuuzilia mbali ripoti kwamba kumekuwepo mawasiliano mapya kati ya Tehran na Washington na kusisitiza kuwa hakuna ujumbe mpya uliowasilishwa kwa Marekani.
-
Bandari ya Chabahar ya Iran kuwa lango la chai na kahawa ya Kenya kuelekea masoko ya Asia ya Kati
Nov 11, 2025 23:10Kenya inatazamia kutumia uwezo wa bandari ya Chabahar ya Iran na kama kitovu cha kanda kwa ajili ya uagizaji na usambazaji wa chai na kahawa.
-
Kwa nini Iran inaunga mkono mamlaka ya kujitawala na umoja wa ardhi ya Sudan?
Nov 11, 2025 07:25Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza uungaji mkono wa Tehran kwa haki ya mamlaka ya kujitawala Sudan.
-
Brigedia Jenerali Belali: Nguvu ya makombora ya Iran imeanza na mizinga
Nov 11, 2025 07:22Mshauri wa Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH amesema: Kitengo cha mizinga cha Iran kiliundwa katika Operesheni Fat'h al-Mobin na baadaye Iran ikafikia kwenye utengenezaji wa makombora. Nguvu yetu ya sasa ni matunda ya miaka minane ya kujihami kutakatifu ambayo yalianzishwa na Hajj Hassan Tehrani-Moghaddam.
-
Araqchi: Magharibi haina chaguo ila kuitambua Iran kama 'kitovu cha sayansi ya nyuklia'
Nov 11, 2025 04:28Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema kuwa nchi za Magharibi hatimaye hazitakuwa na budi ila kuitambua Iran kama kitovu cha kisayansi cha sekta ya amani ya nyuklia.
-
Iran kuzindua satelaiti 3 mwanzoni mwa msimu wa baridi
Nov 11, 2025 04:16Hassan Salarieh, mkuu wa Shirika la Anga za Juu la Iran (ISA) ametangaza mipango ya kurusha kwenye obiti satelaiti tatu zilizoundwa hapa nchini kama sehemu ya jitihada za kuboresha mpango wa anga za juu wa nchi.
-
Kwa nini vikwazo vya mafuta dhidi ya Iran vimefeli?
Nov 10, 2025 23:49Shirika la Kimataifa la Ufuatiliaji wa Meli za Mafuta, katika ripoti yake mpya, limesema kuwa mauzo ya nje ya mafuta ghafi ya Iran yamefikia kiwango cha juu zaidi katika kipindi cha miaka saba iliyopita.