-
Amnesty International yataka mataifa ya Ulaya yaisusie kikamilifu Israel
May 22, 2025 09:21Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International limetoa wito wa kususiwa kabisa utawala wa Kizayuni wakati huu ambapo baadhi ya mataifa ya bara Ulayaa yanachukua hatua za kuutenga utawala huo kutokana na jinai zake huko Gaza.
-
Kombora jingine la Yemen lapiga Tel Aviv mapema leo Alkhamisi
May 22, 2025 02:37Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimeripoti mapema leo Alkhamisi kwamba sauti za ving'ora vya tahadhari zimehinikiza katika maeneo mbalimbali ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni, kufuatia kombora lililorushwa kutoka Yemen ili kupiga maeneo muhimu mno ya Israel.
-
Araqchi: Iran itaendelea kurutubisha urani, kwa makubaliano au bila makubaliano
May 21, 2025 22:58Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi amesema kuwa, Tehran bado haijaamua kama itashiriki katika duru ijayo ya mazungumzo ya nyuklia au la.
-
Kwa nini Uhispania imeongeza mashinikizo dhidi ya Israel?
May 21, 2025 22:48Bunge la Uhispania limepitisha muswada unaoitaka serikali ya nchi hiyo kuacha kuuzia utawala ghasibu wa Israel zana zozote za kijeshi.
-
Wapalestina 26 wamekufa kwa njaa Ghaza katika muda wa saa 24 zilizopita
May 21, 2025 06:41Shirika moja la kimataifa la kutetea haki za binadamu limesema kuwa, takriban Wapalestina 26, wakiwemo watoto wadogo 9, wamekufa kutokana na njaa na ukosefu wa msaada wa matibabu katika Ukanda wa Ghaza unaozingirwa kila upande, kwenye kipindi cha saa 24 zilizopita.
-
Afisa wa Kizayuni: Israel inaua watoto wachanga kwa ajili ya burudani
May 21, 2025 04:00Mkuu wa Chama cha Democrats cha Israel amekosoa jinai za kivita za utawala wa Kizayuni na kusema: "Israel inaua watoto wachanga kwa ajili ya kujifurahisha, na mwenendo huu unaonyesha kutengwa na kukataliwa kwa utawala huo kimataifa."
-
Yemen yaiwekea mzingiro Bandari ya Haifa ili kuiunga mkono Palestina
May 20, 2025 22:56Yemen imetangaza habari ya kuifunga Bandari ya Haifa katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na kupachikwa jina bandia la Israel, ili kuwaunga mkono wananchi wa Palestina na kujibu mashambulizi yanayoendelea kufanywa na Wazayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Ghadhabu za asasi za Marekani kutokana na kushadidi jinai za Israel Ukanda wa Gaza
May 20, 2025 22:55Sisitizo la utawala ghasibu wa Israel la kuendeleza vita vya kutisha vya Gaza katika mwezi wake wa ishirini na mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina, kuitumia njaa kama silaha na kuunda baa la njaa bandia huko Gaza kumepelekea kuibuka radiamali za kimataifa ikiwemo ndani ya Marekani.
-
Jinai za Israel ni kubwa mpaka UK, Canada na Ufaransa zatishia kuiwekea vikwazo
May 20, 2025 03:24Jinai za utawala wa Kizayuni ni kubwa mno na hazivumiliki kiasi kwamba hata viongozi wa Uingereza, Canada na Ufaransa wametishia kuiwekea vikwazo Israel kutokana na uhalifu wa kivita na jinai za kutisha huko Ghaza. Tishio hilo limezidisha mashinikizo kwa nduli wa Ghaza, yaani waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu.
-
Israel yaendeleza mashambulio ya kiwendawazimu Ghaza
May 20, 2025 03:24Duru za habari za ndani ya Palestina zimeripoti mapema leo Jumanne kwamba ndege za kivita za Israel zimefanya mashambulizi makali na ya kiwendawazimu katika maeneo mbalimbali ya mji wa Ghaza.