-
Hamas yaitisha maandamano ya 'mshikamano wa kimataifa' kulaani jinai za Israel Gaza
Apr 16, 2025 23:01Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imetoa wito wa dharura kwa watu wa dunia kushiriki kikamilifu katika maandamano ya wiki moja ya kushinikiza kusitishwa kwa kampeni ya kutisha ya Israel ya mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza.
-
Saudi Arabia yaanzisha tena mashambulizi dhidi ya Yemen?
Apr 16, 2025 23:00Vyanzo vya ndani nchini Yemen vimeripoti habari ya kujiri mashambulizi ya mizinga na makombora ya Saudi Arabia dhidi ya nchi hiyo jirani yake.
-
Makumi ya wanawake, watoto wauawa na mabomu ya Wazayuni Gaza
Apr 16, 2025 11:21Mashambulizi makali ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel yameua shahidi zaidi ya Wapalestina 20, wakiwemo wanawake na watoto wadogo katika Ukanda wa Gaza.
-
Serikali ya Al-Jolani Syria kuanzisha uhusiano rasmi na Israel mwishoni mwa 2026
Apr 16, 2025 08:02Mwanadiplomasia mmoja wa Uingereza amefichua kuwa kiongozi wa kundi la wanamgambo la Hay-at Tahrir al-Sham HTS Abu Mohammed al-Jolani ameihakikishia Uingereza kwamba Syria "itaanzisha uhusiano rasmi wa kidiplomasia" na utawala wa Kizayuni wa Israel, itautambua utawala huo, na kubadilishana nao mabalozi ifikapo mwisho wa mwaka ujao wa 2026.
-
UAE imeweka mtambo wa rada wa Israel Puntland kwa ajili ya kutungua makombora ya Yemen
Apr 16, 2025 08:01Duru za habari zimeripoti kuwa Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE) au Imarati imeweka mtambo wa rada wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi ya Puntland, Somalia ili kuyanasa na kuyatungua makombora yanayorushwa na Yemen.
-
Wazayuni waendeleza mashambulizi Ukingo wa Magharibi, wamjeruhi mtoto Mpalestina
Apr 16, 2025 04:17Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameendeleza mashambulizi na hujuma zao za mara kwa mara katika maeneo mbalimbali ya Ukingo wa Magharibi na kumjeruhi kwa risasi mtoto wa kike wa Kipalestina.
-
Mgogoro mkubwa katika jeshi la Israel; Kwa nini wanajeshi wa utawala huo wanatoroka?
Apr 15, 2025 23:12Barua ya malalamiko ya marubani wa Jeshi la Anga la Israel na uungaji mkono wa askari wa vitengo vingine kwa hatua hiyo ni kengele ya hatari kuhusu uwezekano wa kuenea uasi miongoni mwa wanajeshi wa utawala wa Kizayuni.
-
Walowezi 1000 wa Kizayuni wavamia Msikiti wa Al-Aqsa huku wakilindwa na wanajeshi wa Israel
Apr 15, 2025 22:51Katika siku ya tatu ya sikukuu ya pasaka ya Kiyahudi, walowezi elfu moja wa Kizayuni, huku wakisindikizwa na kupewa ulinzi na wanajeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamevamia eneo la Msikiti mtukufu wa Al-Aqsa katika mji wa Baitul-Muqaddas Mashariki unaokaliwa kwa mabavu.
-
Idadi ya vifo Gaza yafikia 51,000 huku Israel ikiendelea na mashambulizi ya kinyama
Apr 15, 2025 06:47Mashambulizi ya anga ya utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza yamewaua Wapalestina wengine wasiopungua 17 katika saa 24 zilizopita, na hivyo kufanya idadi ya vifo kutokana na vita vya kinyama vya Israel vilivyoanza Oktoba 2023 kufikia 51,000.
-
Mkuu wa majeshi ya Israel akiri: Hamas haijashindwa vitani
Apr 15, 2025 04:00Mkuu mpya wa jeshi la Israel ameonya kuwa, vikosi vya jeshi la utawala huo wa Kizayuni vinakosa nguvu kazi na rasilimali za kutimiza malengo ya kujitanua ya utawala huo katika Ukanda wa Gaza uliozingirwa, na kusema kuwa Hamas inaendelea kuudhibiti ukanda huo, mwaka mmoja na nusu baada ya kuzuka kwa vita hivyo.