-
Viongozi wa Misri na Qatar wakaribisha mazungumzo ya Iran na Marekani nchini Oman
Apr 14, 2025 23:46Rais wa Misri na Amir wa Qatar wametoa taarifa baada ya mazungumzo yao huko Doha, mji mkuu wa Qatar na kukaribisha mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani huko Oman.
-
Iraq yaonya dhidi ya kuibuka upya ISIS nchini Syria
Apr 14, 2025 09:36Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fuad Hussein ameonya kuhusu kushadidi harakati za kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) katika nchi jirani ya Syria, kufuatia kuanguka kwa serikali ya Rais Bashar al-Assad mwishoni mwa mwaka jana.
-
Kushindwa mhimili wa vita wa Kizayuni na Marekani katika vita huko Yemen na Gaza
Apr 14, 2025 07:29Licha ya mashambulizi yanayoendelea kufanywa na mhimili wa Kizayuni na Marekani dhidi ya Yemen na Gaza, bado vikosi vya jeshi la Yemen na Muqawama wa Palestina vinaendelea kukabiliana na wavamizi hao.
-
Jinai za kinyama za Israel Ghaza hazina udhibiti, Wapalestina wengine 37 wauawa shahidi
Apr 14, 2025 02:42Mashambulio makubwa na ya kinyama yaliyofanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika maeneo mbalimbali ya Ghaza yamewaua shahidi Wapalestina wengine wasiopungua 37.
-
Abu Ubaidah: Wapalestina hawatosahau Wayemen walivyosimama nao bega kwa bega
Apr 14, 2025 02:41Msemaji wa Brigedi za Izzuddinul-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema, Wapalestina hawatosahau namna Wayemen walivyosimama imara na bega kwa bega pamoja nao katika Jihadi ya kuikomboa ardhi ya Palestina.
-
Jeshi la Yemen laangusha ndege ya 19 ya kivita ya Marekani
Apr 13, 2025 23:30Jeshi la Yemen limetangaza kuangusha tena ndege ya kisasa ya kivita isiyo na rubani aina ya MQ-9 ya Jeshi la Marekani katika anga ya nchi hiyo.
-
Hamas: Madai ya adui kuhusu hospitali ya Al Mamadani ni uongo unaorudiwa
Apr 13, 2025 22:52Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imetoa tamko kujibu madai ya uongo ya jeshi katili la adui Israel kuhusu kuripuliwa hospitali ya Baptist huko Gaza, na kuyataja madai hayo kuwa ni "uongo unaorudiwa" wa kujaribu kuhalalisha jinai za kivita za utawala ghasibu wa Kizayuni.
-
Jamii ya kimataifa yaendelea kunyamazia kimya jinai za Israel
Apr 13, 2025 08:56Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limetoa onyo kali kuhusu vifo vya watoto wa Gaza kwa wingi kutokana na njaa kali na ukosefu wa chakula.
-
Waislamu wauawa India katika maandamano ya kupinga Sheria ya Marekebisho ya Wakfu wa Kiislamu
Apr 13, 2025 07:58Watu watatu, akiwamo mtoto mmoja, wameuawa na wengine zaidi ya 100 kukamatwa wakati wa maandamano yaliyofanyika katika jimbo la mashariki mwa India la West Bengal kupinga marekebisho ya Sheria ya Bodi za Wakfu wa Kiislamu.
-
Taasisi ya Palestina: Jamii ya kimataifa isaidie sekta ya afya na tiba ya Gaza
Apr 13, 2025 07:18Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imelaani jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuishambulia Hospitali ya Al Maamadani na kuitaka jamii ya kimataifa kuisaidia sekta ya afya na tiba ya eneo hilo.