-
Jamii ya kimataifa yaendelea kunyamazia kimya jinai za Israel
Apr 13, 2025 08:56Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limetoa onyo kali kuhusu vifo vya watoto wa Gaza kwa wingi kutokana na njaa kali na ukosefu wa chakula.
-
Waislamu wauawa India katika maandamano ya kupinga Sheria ya Marekebisho ya Wakfu wa Kiislamu
Apr 13, 2025 07:58Watu watatu, akiwamo mtoto mmoja, wameuawa na wengine zaidi ya 100 kukamatwa wakati wa maandamano yaliyofanyika katika jimbo la mashariki mwa India la West Bengal kupinga marekebisho ya Sheria ya Bodi za Wakfu wa Kiislamu.
-
Taasisi ya Palestina: Jamii ya kimataifa isaidie sekta ya afya na tiba ya Gaza
Apr 13, 2025 07:18Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imelaani jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuishambulia Hospitali ya Al Maamadani na kuitaka jamii ya kimataifa kuisaidia sekta ya afya na tiba ya eneo hilo.
-
Hamas: Shambulio la Israel katika Hospitali ya Kibaptisti ni uhalifu wa kivita kwa msaada wa Marekani
Apr 13, 2025 03:25Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa, kulipuliwa kwa Hospitali ya Kibaptisti katika mji wa Gaza, kuharibiwa jengo la mapokezi na huduma za dharura na kutimuliwa wagonjwa na majeruhi ni uhalifu mpya wa kivita uliofanywa na jeshi la Israel kwa baraka za Marekani ikiwa ni sehemu ya uhalifu wa kikatili unaoendelea kufanywa katika Ukanda wa Gaza.
-
Nakala adimu ya Qur’ani katika Msikiti wa Al-Aqsa, iliandikwa na mjukuu wa Mtume
Apr 12, 2025 22:52Jumba la Makumbusho ya Kiislamu katika Msikiti wa Al-Aqsa, Quds Tukufu (Jerusalem) inayokaliwa kwa mabavu, lina idadi ya vitabu adimu, ikiwa ni pamoja na nakala ya kipekee ya Qur’ani iliyoandikwa kwa hati za Kufi, ambayo mwisho wake inaeleza kuwa iliandikwa na Al-Hasan bin Al-Hussen bin Ali bin Abi Talib (as), mjukuu wa Mtume Muhammad, (saw).
-
UN: Wapalestina 400,000 Gaza wamefurushwa makwao ndani ya wiki 3
Apr 12, 2025 08:10Takwimu mpya za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa, idadi kubwa ya Wapalestina wamelazimika kuyahama makazi yao katika Ukanda wa Gaza tangu utawala haramu wa Israel uanzishe mashambulizi mapya baada ya kuvunja makubaliano ya usitishaji vita zaidi ya wiki tatu zilizopita.
-
Kwa mara nyingine Yemen yayatwanga maeneo ya jeshi la Israel huko Jaffa
Apr 12, 2025 03:11Jeshi la Yemen (YAF) limetangaza habari ya kufanya operesheni nyingine ya ndege zisizo na rubani na kutwanga maeneo mawili ya jeshi la Israel katika eneo Jaffa karibu na Tel Aviv na kusema kuwa hayo ni majibu ya moja kwa moja ya mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina huko Ghaza.
-
UN: Mashambulio 36 ya Israel Ghaza kati ya Machi 18 hadi Aprili 9 yameua wanawake na watoto tu
Apr 11, 2025 23:38Umoja wa Mataifa umesema wanawake na watoto wa Kipalestina ndio pekee waliouawa katika mashambulizi yapatayo 36 ya anga yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza tangu katikati ya mwezi Machi na kuonya kwamba mashambulizi ya kijeshi ya Israel yanahatarisha "kuendelea kuwepo Wapalestina kama jamii".
-
Mamilioni waandamana Yemen kuunga mkono Ghaza
Apr 11, 2025 07:28Mamilioni ya wananchi wa Yemen wamemiminika mitaani katika mkoa wa Sa'ada leo Ijumaa na kufurika katika viwanja 35 vya mkoa huo wa kaskazini ya Yemen chini ya kaulimbiu ya "Jihadi, Uthabiti na Ushujaa... Hatutaiacha peke yake Ghaza."
-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina yapongeza uamuzi wa Macron kuitambua rasmi Palestina
Apr 11, 2025 04:10Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imekaribisha msimamo uliotangazwa na Rais wa Ufaransa kuhusu uwezekano wa nchi hiyo kulitambua rasmi Taifa la Palestina katika miezi ijayo.