-
Kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Wanawake: Zaidi ya wanawake 12,000 wa Kipalestina wameuawa katika vita vya Gaza
Mar 08, 2025 09:24Idara ya Habari ya Serikali ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa: Wanawake 12,316 wa Kipalestina wameuawa shahidi katika vita vya mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni Israel dhidi ya watu wa Gaza.
-
Sasa Trump ameelewa, HAMAS haimuogopi
Mar 08, 2025 07:51Mchambuzi mmoja mashuhuri wa ulimwengu wa Kiarabu amesema: "Kulazimika Donald Trump kuomba kufanya mazungumzo ni matokeo ya kufeli na kukata tamaa serikali yake katika njama zake za kuilazimisha Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS itii amri zake.
-
OIC yalaani njama za kuhamishwa kwa nguvu Wapalestina Ghaza
Mar 08, 2025 07:51Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imetoa taarifa rasmi mwishoni mwa kikao chake cha mjini Jeddah, Saudi Arabia na kulaani kwa nguvu zote njama za Marekani na Israel za kutaka kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza.
-
Nini kinaendelea Syria? Taasisi za kimataifa kimya!
Mar 08, 2025 07:47Ukimya wa taasisi za kimataifa kuhusiana na mauaji ya umati dhidi ya raia nchini Syria yanayofanywa na viongozi wenye mafungamano na utawala wa al-Julani kwa mara nyingine tena unathibitisha undumilakuwili wa taasisi hizo.
-
Askari wa Israel wavamia misikiti mjini Nablus na kuzuia Swala ya Ijumaa
Mar 07, 2025 07:31Vikosi vya jeshi la Israel vimevamia misikiti kadhaa katika mji mkongwe wa Nablus, eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kuzuia kuswaliwa Swala ya Ijumaa.
-
70 wauawa katika mapigano baina ya pande kinzani Syria
Mar 07, 2025 07:28Zaidi ya watu 70 wameripotiwa kuuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa nchini Syria kutokana na mapigano makali kati ya wanamgambo wa kundi la kigaidi linalotawala la Hay’at Tahrir al-Sham (HTS) na makundi ya Muqawama ya wananchi huko magharibi mwa nchi hiyo.
-
Jeshi la Israel launda kifaa cha AI cha kuwajasisi Wapalestina
Mar 07, 2025 07:27Uchunguzi mpya umefichua kuwa, kitengo cha ujasusi wa kielektroniki cha jeshi la Israel cha 8200 kimetumia mkusanyiko mkubwa wa mawasiliano yaliyonaswa kutengeneza chombo cha kijasusi cha Akili Mnemba (AI) ambacho modeli yake inashabihiana na ChatGPT, kwa lengo la kuwachunguza na kuwafanyia ujasusi wananchi wa Palestina.
-
Netanyahu awazidishia vizuizi Wapalestina vya kusali Ijumaa Msikiti wa Al-Aqsa mwezi wa Ramadhani
Mar 07, 2025 04:05Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu ameidhinisha vizuizi vikali vya kuwekewa Waislamu Wapalestina kuingia katika Msikiti wa Al-Aqsa kwa ajili ya Sala ya Ijumaa wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
HAMAS yasema imejiandaa 'kwa chochote kitachotokea' baada ya 'onyo la mwisho' alilotoa Trump
Mar 07, 2025 00:02Brigedi za Izzuddinul-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS zimetangaza kwamba, zimejiandaa kwa "chochote kitachotokea" na zingali ziko kwenye hali ya "tahadhari kamili", zikisisitiza kuwa, vitisho vya utawala wa Kizayuni wa Israel vya kuanzisha tena vita dhidi ya Ukanda wa Ghaza havitatoa hakikisho kwa utawala huo dhalimu la kuweza kuwakomboa mateka wake.
-
Yemen: US kuiweka Ansarullah katika orodha ya ugaidi haina uhalali wowote
Mar 06, 2025 23:03Afisa mmoja mwandamizi wa Yemen amepuuzilia mbali hatua ya Marekani ya kuitambua Harakati ya Muqawama ya Ansarullah kama kundi la kigaidi, akisema uamuzi huo hauna uhalali wowote.