-
Mpasuko Israel, Smotrich ajiondoa katika utawala wa Netanyahu
Apr 01, 2025 04:12Waziri wa Fedha wa utawala haramu wa Israel, Bezalel Smotrich, ametangaza kujiuzulu kutoka wadhifa wake, jambo ambalo linaongeza matatizo ndani ya serikali ya muungano ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.
-
Jeshi la Yemen laangusha ndege ya kivita ya Marekani aina ya MQ-9
Mar 31, 2025 23:37Jeshi la Yemen limetangaza kuangusha ndege ya kivita ya isiyo na rubani au droni ya Marekani aina ya MQ-9 katika Mkoa wa Ma’rib, ikiwa ni droni ya 16 kuangushwa na nchi hiyo tangu Oktoba 7, 2023.
-
ICRC: Tumeshtushwa na jinsi Israel inavyofanya jinai bila ya kiwewe
Mar 31, 2025 23:18Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (ICRC) limesema kuwa, limeshtushwa na jinsi utawala wa Kizayuni wa Israel unavyofanya jinai za kutisha huko Ghaza bila ya hofu wala kiwewe.
-
Iran yasisitizia kuharakishwa utekelezaji wa makubaliano kati yake na Qatar
Mar 31, 2025 23:17Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na Amir wa Qatar na kutilia mkazo wajibu wa kuharakishwa utekelezaji wa makubaliano kati ya nchi hizo mbili na kuimarishwa uhusiano wa kirafiki na ujirani mwema.
-
Utawala wa Kizayuni waendelea kupinga utoaji wa misaada kwa Wapalestina
Mar 31, 2025 06:43Vitendo vya kikatili vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wanaoishi Gaza vinaendelea, na bado utawala huo unazuia kufikishwa kwa misaada ya chakula na dawa kwa wakazi wa Gaza.
-
Jinai za kinyama za Israel za kuwaua Wapalestina hata katika Siku ya Idi zalaaniwa vikali
Mar 31, 2025 04:11Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeendelea kuwaua watu wa Ghaza hata katika wakati huu wa Sikukuu ya Idul-Fitri na kutoonyesha heshima yoyote kwa Sikukuu hiyo.
-
Kiongozi mwandamizi wa HAMAS: Muqawama na Silaha zake, kwetu sisi ni mstari mwekundu
Mar 31, 2025 03:29Bassem Naim, kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: "kwetu sisi tukiwa ni taifa linalokaliwa kwa mabavu, Muqawama na silaha zake ni mstari mwekundu na ni suala la uwepo wetu na uhai wetu".
-
Televisheni ya Israel: Mashambulio ya Marekani hayana athari yoyote dhidi ya operesheni za Yemen
Mar 31, 2025 03:29Televisheni ya utawala wa Kizayuni wa Israel imekiri kuwa, mashambulizi ya Marekani ya kuzuia operesheni zinazofanywa na Yemen dhidi ya utawala huo wa Kizayuni hazijawa na athari yoyote.
-
Jeshi la Yemen laendelea kuzitwanga kwa makombora meli za kivita za Marekani
Mar 30, 2025 07:42Jeshi la Yemen limetangaza kuhusika na mfululizo wa mashambulizi yaliyofanyika kwa ustadi wa hali ya juu na kuzitwanga meli za kivita za Marekani, ikiwa ni pamoja na USS Harry S. Truman, katika Bahari Nyekundu, ikiwa ni kuendelea kukabiliana na uvamizi wa Marekani dhidi ya Yemen.
-
Ujumbe wa HAMAS wa Sikukuu ya Idul Fitr
Mar 30, 2025 07:41Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa ujumbe wa Sikukuu ya Idul Fitr kwa kuyataka mataifa ya Kiislamu na Kiarabu kuongeza juhudi na uungaji mkono kwa Wapalestina ili kukomesha jinai za Israel na kuondolewa mzingiro kwenye Ukanda wa Ghaza.